Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, August 17, 2016

AZAM FC YAIGARAGAZA YANGA KWENYE NGAO YA JAMII



NI kama gari inayopata pancha huku dereva akikaribia kufika safari yake. Ndivyo ilivyotokea kwa Yanga le ilipotema kombe la kwanza  baada ya kufungwa na Azam kwa mikwaju ya penalti 4-1 katika mechi ya Ngao ya Jamii iliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Ikiwa imeshahesabu ushindi baada ya kuongoza kwa mabao 2-1 katika dakika 90 za mchezo huo, Yanga ilijikuta matatani baada ya Azam kusawazisha bao dakika ya 90 na kulazimika kwenda kwenye mikwaju ya penalti baada ya kutoka sare ya mabao 2-2.
Mechi hiyo ni ya kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu bara ambayo msimu huu wa mwaka 2016/2017 unaanza keshokutwa.
Yanga imetema kombe hilo ililolitwaa mwaka jana baada ya kuifunga Azam kwa mikwaju ya penalti 8-7. Timu hiyo bado inashikilia ubingwa wa kombe la FA na wa Ligi Kuu.
Wachezaji Ramadhan Kessy aliyecheza Yanga kwa mara ya kwanza na Haruna Niyonzima ndio waliokosa penalti ambapo Kessy penalti yake kuokolewa na kipa wa Azam Aishi Manula huku Niyonzima kupiga juu. Kipa wa Yanga Deogratius Munishi ‘Dida’ ndiye aliyepata penalti kwa upande wa Yanga.
Penalti za Azam zilifungwa na  Bocco, Himid Mao,Kapombe na Michael Balou.
Yanga ilianza kwa kasi mechi hiyo na ilionekana kuwa na kila dalili ya kuibuka na ushindi hasa baada ya Azam kuonekana kutojiweza karibu dakika zote za kipindi cha kwanza.
Mshambuaji wa kimataifa wa Zimbabwe, Donald Ngoma aliindikia Yanga bao la kuongoza katika dakika ya 18 kwa mkwaju wa penalti iliyotolewa na mwamuzi Ngole Mwangole wa Mbeya baada ya Ngoma kufanyiwa madhambi eneo la hatari na Shomari Kapombe.
Dakika moja baadae Ngoma aliandika bao lingine baada ya kuunganisha krosi ya Amisi Tambwe na kuujaza mpira wavuni.
Bao hilo lilizidi kuwachanganya Azam ambapo sasa wachezaji wake walionekana kupoteana zaidi lakini walihimili kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao hayohayo.
Azam ambayo haikupewa nafasi kubwa kushinda mechi ya jana kutokana na kukosa matokeo mara kwa mara wanapokutana na Yanga, ilianza kipindi cha pili kwa mabadiliko ambapo walimtoa Shaaban Chilunda na Ramadhan Singano na nafasi zao kuchukuliwa na Francisco Zekumbariwa na Mudathir Yahaya, mabadiliko yaliyoonekana kuzaa matunda kwani sasa ilibadilika na kuanza kupeleka mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwa Yanga.
Dakika ya 75 Kapombe aliisawazishia Azam bao la kwanza baada ya kuunganisha pasi ya Jean Mugiraneza na kuujaza mpira wavuni.
Dakika ya 90 John Bocco aliisawazishia Azam bao la pili kwa mkwaju wa penalti iliyotolewa na mwamuzi baada ya beki wa Yanga kushika mpira eneo la hatari.
mwisho.


No comments:

Post a Comment