Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, December 26, 2015

YANGA YAZIDI KUJIWEKA KILELENI WAKATI SIMBA YAENDELEZA SARE






YANGA  imezidi kuchanja mbuga  kuelekea kutetea taji lake la Ligi Kuu baada ya jana kuifunga Mbeya City mabao 3-0.

Ushindi huo umeifanya Yanga ifikishe pointi 33 kwenye msimamo ikiwa kileleni.

Mshindani wake katika kuwania taji hilo ni Azam ambayo haijacheza mechi mbili ikiwa na pointi 29.

Azam leo inacheza na Kagera Sugar, na ikishinda itaikaribia zaidi Yanga. Azam imecheza michezo pungufu mpaka sasa.

Amisi Tambwe alikuwa shujaa wa Yanga jana baada ya kuifungia mabao mawili huku moja likifungwa na Thaban Kamusoko.

Tambwe alifunga bao la kwanza katika dakika ya 36 kwa shuti kali baada ya kuunganisha pasi nzuri ya Simon Msuva.

Tambwe tena alicheka na nyavu kufunga bao la pili katika dakika ya 65 kwa krosi ya Haji Mwinyi.
 Dakika moja baadaye Thaban Kamusoko alifunga bao la tatu akitengenezewa na Msuva tena.

Mechi hiyo ilipooza kipindi cha kwanza kabla ya kuchangamka katika kipindi cha pili huku Yanga wakionekana kuutawala mchezo.
Kutoka kwenye uwanja wa Kambarage Shinyanga Simba imeendelea kutoa sare baada ya kutoka 1-1 na Mwadui.
Hiyo ni sare ya tatu kwa Simba baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Azam, na 1-1 na Toto Africans. Mwadui ndio ilikuwa ya kwanza kupata bao lililofungwa na Nizar Khalfani kabla Simba haijasawazisha kupitia kwa mchezaji wake Brian Majwega.

Kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona Mtwara Ndanda ya huko nayo iliendelea kugawa pointi baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa JKT Ruvu.
Majimaji ya Songea, ikiwa nyumbani uwanja wa Majimaji iliangukia pua kwa kuchapwa mabao 2-0 na Prisons huku Mtibwa Sugar ikitumia vyema uwanja wake wa Manungu kwa kuichapa Mgambo JKT mabao 3-0.
Kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga, wagosi wa Kaya Coastal Union walipigwa mabao 3-1 na Stand United.


No comments:

Post a Comment