Zipo habari zinazodai kuwa Louis van Gaal atapewa Mechi 2 zijazo kurekebisha mwelekeo wa jahazi lakini zipo dalili pengine hata huo muda haupo.


Mechi zijazo za Ligi:
Desemba 26: Stoke City vs Man United
Desemba 28: Man United vs Chelsea
Januari 2: Man United vs Swansea City

Wapo wanaosema Van Gaal atang’oka na Msaidizi wake Ryan Giggs kupewa ukaimu hadi mwishoni mwa Msimu na Giggs akifanya vizuri katika kipindi cha ukaimu hapo ndipo atakuwa wa kudumu .
Lakini pia zipo taarifa zinazodai Jose Mourinho, alietimuliwa na Chelsea Alhamisi iliyopita, ndie atashika wadhifa wa Umeneja wakati wowote kuanzia sasa.
Hadi sasa hamna mwenye uhakika nini kitajiri Man United na Klabu yenyewe haijazungumza chochote kama kawaida yao.


No comments:
Post a Comment