Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, December 29, 2015

LEICESTER vs MANCHESTER CITY, NANI KUIBUKA KIDEDEA?

Patashika za Ligi Kuu England kuendelea tena leo, Kuna Mechi moja pekee ambayo itaamua nani anamaliza 2015 akiwa anaongoza Ligi.
Jana, Arsenal iliichapa Bournemouth 2-0 na kutwaa uongozi wa Ligi wakiwa na Pointi 39 kwa Mechi 19 wakifuata Leicester wenye Pointi 38 kwa Mechi 18, Tottenham ni wa 3 na wana Pointi 35 kwa Mechi 19 na wa 4 ni Man City wenye Pointi 35 kwa Mechi 18.
Leo huko King Power Stadium, Leicester wanacheza na Man City na wakishinda watarudi kileleni na wakitoka Sare watabaki Nafasi ya Pili.
Ikiwa City itashinda basi watapanda hadi Nafasi ya Pili.
Leicester wanatinga kwenye Mechi hii wakitoka kufungwa 1-0 na Liverpool na kupoteza wimbi lao la kutofungwa katika Mechi 10 wakati City ikiichapa Sunderland 4-1.
Wakati Leicester wana Kikosi kamili bila Majeruhi ingawa mapema walipatwa na wasiwasi wa Staa wao Jamie Vardy, ambae ndie Mfungaji Bora wa Ligi, kutocheza kutokana na kuugua, City watamkosa Nahodha wao Vincent Kompany ambae ni Majeruhi pamoja na majeruhi wengine Pablo Zabaleta, Fernando na Samir Nasri.
Yaya Toure kendeleza tena wimbi la mabao

No comments:

Post a Comment