Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, December 31, 2015

Hakuna anayewaza ubingwa – Ranieri

2AB2DC0500000578-0-image-a-39_1437405095039

Kocha wa Leicester City, Claudio Ranieri (pichani) amesema bado hawawezi kubashiri kama wanaweza kuibuka mabingwa wa Ligi Kuu ya Wingereza na hakuna anayewaza hilo ndani ya kikosi chake.
Ranieli ameyasema hayo baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi ya Uingereza kati ya Leicester City iliyowakaribisha Manchester City ambapo mchezo huo ulimalizika kwa sare ya bila kufunguna kwa timu hizo.
Alisema kuwa ligi ya Wingereza imekuwa haitabiriki unaweza kuwa katika kiwango kizuri lakini hali ikabadilika na nafasi ikachukuliwa na timu nyingine ambayo akafanikiwa na kuchukua ubingwa.
“Hii ligi inashangaza sana, nadhani timu kubwa zinaweza kuwa katika kiwango cha juu lakini muda mwingine hakuna mtu anataka kushinda ligi, mambo yanabadilika katika ligi hii,
“Sio rahisi kwetu lakini tunataka kupambana na kila mtu, ni maajabu haya tunayoyafanya,” alisema Ranieli.
Aidha Ranieli amesema anaridhishwa na kasi waliyonayo wachezaji wake na kwake limekuwa jambo la kushangaza kutokana na kasi waliyonayo na anatumai kuwa kasi hiyo itaendelea kuwepo na watafika mbali zaidi.
Leicester kwa sasa wamefikisha alama 40 wakiwa katika nafasi ya pili nyuma ya Arsenal ambao wanalingana nao alama na Arsenal ikiwa imewashinda Leicester magoli ya kufungwa na kufunga.
Msimu uliopita hadi kumaliika kwa mwaka 2014 kuingia 2015, Leicester City ilikuwa katika nafasi ya mwisho ya msimamo wa Ligi Kuu ya Wingereza lakini kunaonekana kuwapo na mabadiliko makubwa katika klabu hiyo baada ya kumchukua Ranieli kuwa meneja wa klabu na sasa inaonekana kuwa na mafanikio makubwa.

No comments:

Post a Comment