Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, December 8, 2015

DROO YA RAUNDI YA 3 YA FA CUP, YAPANGWA, MABINGWA ARSENAL KUCHEZA NA SUNDERLAND NYUMBANI EMIRATES, MAN UNITED v SHEFFIELD UNITED, CHELSEA v LEYTON ORIENT/ SCUNTHORPE.

DROO ya Raundi ya 3 ya Kombe kongwe Duniani, FA CUP, ambalo sasa linaitwa Emirates FA Cup kwa sababu za kiudhamini, imefanyika Usiku huu ikihusisha Timu zote za Ligi Kuu England na Daraja la Championship ambazo huanzia hapa.
Droo hii, ambayo imeibua Mechi 5 za Timu za Ligi Kuu England kuvaana wenyewe kwa wenyewe, imefanyika huko Sport Wales National Centre Mjini Cardiff, na kuhusisha Timu 64 na Mechi zake zitachezwa kati ya Ijumaa Januari 8 na Jumatatu Januari 11.

Arsenal, ambao ndio Mabingwa Watetezi baada ya kulitwaa Kombe hili kwa mara ya pili mfululizo Mwezi Mei Mwaka huu, watakuwa kwao Emirates kucheza na Sunderland wakati Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, Chelsea, wapo kwao Stamford Bridge kucheza na Mshindi kati ya Timu za Madaraja ya chini Leyton Orient v Scunthorpe United.
Manchester United wapo kwao Old Trafford kucheza na Sheffield United wakati Man City wako Ugenini kucheza na Norwich City.
Liverpool wako Ugenini kuivaa Exeter City huku Mechi tamu iko White Hart Lane ambako Tottenhma watavaa Vinara wa Ligi Kuu England Leicester City. 

Droo ya Raundi ya Tatu:
Watford v Newcastle
West Brom v Bristol City
West Ham v Wolves
Salford/Hartlepool v Derby
Exeter City v Liverpool
Northampton Town v MK Dons
Peterborough v Preston
Colchester v Charlton
Tottenham v Leicester
Arsenal v Sunderland
Ipswich Town v Portsmouth
Newport County v Blackburn Rovers
Sheffield Wednesday v Fulham
Wycombe Wanderers v Aston Villa
Birmingham City v AFC Bournemouth
Oxford United v Swansea City
Brentford v Chesterfield or Walsall
Bury v Bradford City
Manchester United v Sheffield United
Everton v Dagenham and Redbridge/Whitehawk
Southampton v Crystal Palace
Carlisle United v Yeovil Town
Nottingham Forest v QPR
Eastleigh v Bolton Wanderers
Chelsea v Leyton Orient/Scunthorpe United

Doncaster Rovers v Stoke City
Leeds United v Rotherham United
Huddersfield v Reading
Cardiff City v Grimsby Town/Shrewsbury Town
Norwich City v Manchester City
Middlesbrough v Burnley
Hull City v Brighton and Hove Albion

THE EMIRATES FA CUP 2015/16
TAREHE MUHIMU
Raundi ya 3
Jumamosi 9 Januari 2016
Raundi ya 4
Jumamosi 30 Januari 2016
Raundi ya 5
Jumamosi 20 Februari 2016
Raundi ya 6-Robo Fainali
Jumamosi 12 Machi 2016
Nusu Fainali
Jumamosi 23 Aprili 2016 & Jumapili 24 Aprili 2016
Fainali Jumamosi 21 Mei 2016

No comments:

Post a Comment