Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, July 10, 2015

TANZANITE KUWAKABILI YOUNG SHE-POLOPOLO KESHO

Timu ya Taifa ya Wanawake ya Tanzania wenye umri chini ya miaka 20 (Tanzanite) itashuka dimbani siku ya jumamosi katika uwanja wa Azam Complex kucheza na timu ya U20 ya Zambia (The Young She-polopolo) katika mchezo wa kwanza kuwania kufuzu kwa fainali za U-20 za Dunia mwaka 2016.

Mechi kati ya Tanzanite dhidi ya Young She-Polopolo kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 20 itachezwa katika uwanja wa Azam Complex - Chamazi majira ya saa 10 kamili jioni.

Kikosi cha timu ya Tanzanite chini ya kocha wake mkuu Rogasian Kaijage iliyoweka kambi  eneo la Mbande na kufanya mazoezi yake katika uwanja wa Azam Complex kwa takribani wiki ya pili sasa kujiandaa na mchezo huo.

Hali ya kambi ya Tanzanite ni nzuri wachezaji wote wapo katika hali nzuri na morali ya ya hali ya juu, kikubwa Watanzania wanaombwa kujitokeza kwa wingi siku ya jumamosi kuja kuwapa sapoti timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 20 watakapokuwa wakicheza na wenzao wa Zambia.

Nayo timu ya Taifa ya U20 ya Zambia Young She-polopolo inatarajiwa kuwasili kesho alhamis  jioni kwa usafiri wa ndege wa shirika la Rwanda Air ambapo ijumaa wanatarajiwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Azam Complex.

Mchezo huo utachezwa siku ya jumamosi majira ya saa 10 kamili jioni katika uwanja wa Azam Complex - Chamazi, ni wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Dunia za Wanawake chini ya miaka 20 (U-20) zitakzofanyika nchini Papua New Guninea mwaka 2016.

Mwamuzi wa mchezo huo ni Batol Mahjob kutoka nchini Sudan, akisaidiwa na washika kibendera Remaz Osaman na Walaa Bilal, mwamuzi wa akiba Khadmallah Elasayed wote kutoka nchini Sudan na Kamisaa wa mchezo ni Flora Roosevelt kutoka nchini Malawi.

Wakati huo huo Kikundi cha ushangiliaji cha timu za Taifa (Taifa Supporters) kimejiandaa kwenda kuwapa sapoti timu ya Tanzanite siku ya jumamosi katika mchezo dhidi ya The Young She-Polopolo uwanja wa Azam Comlpex.

Taifa Supporters baadaya kikao cha viongozi wa wao wamepanga kuwa na kikundi cha ushangiliaji cha watu wasiopungua 150 (mia moja hamsini) katika mechi hiyo ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Dunia kwa Wanawake chini ya miaka 20.

Wanchama wa kikundi cha Taifa Supporters watakutana jumamosi saa 5 kamili asubuhi kisha kuelekea uwanja wa Azam kwa ajili ya kuwashangilia Tanzanite katika mchezo huo.

Wapenzi wa mpira wa miguu, wadau mnaombwa kujitokeza siku ya jumamosi kuwapa sapoti Tanzanite katika mchezo wao wa awali dhidi ya Zambia, kabla ya mchezo wa marudaino utakaofanyika tarehe 25 Julai, 2015  Lusaka nchini Zambia.

No comments:

Post a Comment