Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, June 27, 2015

WACHEZAJI WA SIMBA WACHEKELEA UJIO WA KOCHA KERR







WACHEZAJI Simba wachekelea ujio wa kocha mpya Muingereza Dylan Kerr aliyewasili jana tayari kuanza kazi ya kukinoa kikosi hicho kwa msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Akizungumza baada ya mazoezi yaliyofanyika kwenye gym ya Chang’ombe jijini Dar es Salaam, Mussa Mgosi alisema wao wamefurahi kusikia kocha amekuja hivyo wapo tayari kumpokea na kumpa ushirikiano.
“Sisi wachezaji kazi yetu ni kucheza mpira hivyo kocha yeyote atakaye letwa tunampokea na tunampa ushirikiano na leo tunalifikiri angekuja tusalimiane naye lakini ndo hivyo hajafika ila tunamkaribisha sana’, alisema Mgosi
Kerr aliwasili jana saa 10 jioni , Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)  na ndege ya Shirika la Emitares na kulakiwa na wajumbe wawili wa kamati ya Simba, Collin Frisch na Said Tully na kuongea na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali waliokuwepo uwanjani.
Kerr amerithi mikoba ya Mserbia Goran Kopunovic,  amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha Simba ambapo atakuwa anasaidiwa na kiungo wa zamani wa timu hiyo Suleman Matola na kocha wa makipa Idd Salim toka Kenya ambaye naye aliwasili juzi.
Simba waliamua kuachana na Kopunovic na kusaka kocha huyo mpya baada ya Mserbia huyo kuhitaji Simba imlipe kiasi cha Dola za Marekani 50,000 (sh. Milioni 100) kama ada ya usajili na mshahara wake ambapo kila mwezi atakuwa analipwa dola za Marekani 14,000 (sh. Milioni 28).
Baada ya kushindwana kwenye malipo ndipo uongozi uliamua kumsaka kocha mpya na kumpata Kerr ambaye inasemekana atalipwa mshahara wa dola za marekani 9,000 sawa na milioni 18 kwa mwezi.

No comments:

Post a Comment