Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, June 27, 2015

CARLOS TEVEZ AJIUNGA RASMI NA KLABU YA KWAO BOCA JUNIORS

Straika wa Argentina Carlos Tevez amekamilisha Uhamisho wake kwenda Boca Juniors kutoka kwa Mabingwa wa Italy Juventus.
Tevez, mwenye Miaka 31, alianzia Soka lake huko kwao na Klabu ya Boca ambayo aliihama Mwaka 2004 kwenda Brazil kuchezea Corinthians na kisha kukaa Miaka 9 akichezea Klabu za Ulaya.
Huko Ulaya alizichezea Klabu za England, West Ham, Mwaka 2006-2007, Manchester United, 2007-2009, na Manchester City, 2009-2013, na kisha kwenda Italy kuichezea Juventus ambako msimu uliopita aliisaidia tena kutetea Taji lao la Ubingwa kwa kupiga Bao 20.
Majuzi Juventus walimbadili Tevez kwa kumsaini Straika wa Atletico Madrid ya Spain, Mario Mandzukic ambae anatoka Croatia.
Alfajiri hii, Tevez alitoa mchango mkubwa kwa Nchi yake Argentina pale alipofunga Penati ya mwisho katika Mechi ya Robo Fainali ya Copa America na kuifikisha Argentina Nusu Fainali baada ya kuibwaga Colombia kwa Penati 5-4 baada ya Sare ya 0-0 katika Dakika 90.
Akithibitisha Uhamisho huu, Rais wa Boca Juniors Daniel Angelici alisema: "Ni Siku ya furaha sana na ya kuridhisha. Kurudi kwa Tevez akiwa kwenye kilele cha mafanikio ni habari njema kwa Washirika na Mashabiki wote wa Boca na Soka la Argentina!"
Tevez, ambae alitwaa Ubingwa mara 3 huko England na mara 2 huko Italy, alifunga Bao 38 katika Mechi 110 alizochezea Boca alipokuwepo huko mara ya kwanza ambako pia alitwaa Ubingwa Mwaka 2003 na kutwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Marekani ya Kusini kwa mara 3 mfululizo.

Tevez alizaliwa akijulikana kama Carlos Alberto Martínez huko Ciudadela Jimbo la Buenos Aires lakini Wazazi wake wakabadili Jina lake na kumpa ubini wa Mama yake kutokana na mfarakano kati ya Klabu yake ya Utotoni All Boys na Boca Juniors.
Tevez alikulia huko Jimbo la Buenos Aires kwenye Kitongoji cha Ejército de Los Andes, maarufu kama "Fuerte Apache".
Na ndio maana Carlos Tevez hujulikana sana huku kwao kama "El Apache".

No comments:

Post a Comment