
Kawaida Fainali ya Kombe hili huchezwa Uwanja usio wa Timu iliyo Fainali lakini baada ya Real Madrid kugomea kutoa Uwanja wao Santiago Bernabeu ukaanza mvutano wa wapi Fainali hiyo ichezwe.

Hatimae Nou Camp ilipita na hii itakuwa mara ya kwanza kwa Timu iliyo Fainali kucheza Fainali Uwanja wake wa Nyumbani tangu 2002 wakati Deportivo La Coruna walipoifunga Real Madrid Nyumbani kwao Santiago Bernabeu.

Ikiwa Barca watatwaa Kombe hili, ambalo wao wanaongoza kwa kulibeba mara nyingi, hii itakuwa mara yao ya 27 wakati Athletic Bilbao wakifuata kwa wingi wa kulitwaa kwa kulichukua mara 23.
No comments:
Post a Comment