FA,
Chama cha Soka England, kimemfungia Sentahafu wa Liverpool Martin
Skrtel Mechi 3 baada ya kumpata na hatia ya kumkanyaga kwa makusudi Kipa
wa Manchester United David De Gea Jumapili iliyopita Uwanjani Anfield
wakati wa Mechi Ligi Kuu England ambayo Liverpool walichapwa 2-1.


Lakini hii Leo Jopo Huru la FA limetupilia mbali utetezi wa Sentahafu huyo na kumfungia Mechi 3 na atazikosa Mechi 2 za Ligi Kuu England za Aprili 4 huko Emirates na Arsenal na ile ya Anfield na Newcastle hapo Aprili 14 na Marudiano ya FA CUP ya Robo Fainali huko Ewood Park na Blackburn Rovers hapo Aprili 8.
Hizo pia ndizo Mechi ambazo Kepteni Steven Gerrard atazikosa baada ya Kadi Nyekundu kwenye Mechi hiyo hiyo aliyolambwa Sekunde 38 tu tangu aingie Uwanjani kutoka Benchi kwa kumkanyaga kwa kusudi Ander Herrera wa Man United.
No comments:
Post a Comment