Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, March 28, 2015

MADA MAUGO AMCHAKAZA KASEBA KWA KO


Bondia Mada Maugo amemaliza ubishi kwa kumtwanga Japhet Kaseba kwa KO.


Maugo amemchapa Kaseba katika raundi ya nane katika pambano lililomalizika muda mfupi uliopita kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar.

Pambano hilo lilikuwa la kumaliza ubishi kati yao na Maugo alitawala raundi mbili za mwanzo, kabla ya Kaseba kutawala raundi ya tatu na nne.

Kaseba alishindwa kuvumilia mapigo ya Maugo baada ya kuchapwa kwa konde kali la kushoto na kuanguka katika raundi ya nane.

Juhudi zake za kuinuka zilishindikana na kumpa ruhusa mwamuzi kumaliza pambano hilo.

Katika pambano jingine, Karama Nyilawila naye alimshinda Ibrahim Tambwe kwa KO katika raundi ya pili.

Na Ashraf naye akammaliza Ally Ramadhani kwa TKO katika raundi ya pili tu.

No comments:

Post a Comment