Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, December 9, 2014

TAIFA STARS YA MABORESHO (TANZANIA) YAFUNGWA NA U-23 YA BURUNDI TAIFA LEO








KIKOSI cha timu ya taifa ya maboresho leo kimefungwa mabao 2-1 na timu ya vijana chini ya umri wa miaka 23 ya Burundi katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliofanyika kwenye uwanja wa taifa Dar es Salaam.
Katika mchezo  huo timu zote mbili zilianza mpambano huo kwa kasi huku kila upande ukisoma mbinu za wapinzani wao ili kuweza kupata bao la mapema.
Vijana wa Tanzania ndio waliokuwa wa kwanza kulifikia lango la wageni wao Burundi na kupoteza nafasi ya wazi kupitia kwa mshambuliaji wake Kelvin Friday ambaye katika mchezo huo alionekana kutokuwa makini kwa kupoteza nafasi nyingi alizozipata.
Kufuatia kosakosa hizo za vijana wa maboresho Burundi wanao nolewa na kocha Mjerumani  Wilfried Rainer, walitulia na kupanga vyema mashambulizi yao lakini walijikuta wakifungwa bao la mapema na mshambuliaji Rashidi Yusufu aliyefunga kwa kichwa akiunganisha krosi ya Gidaeli Michael.
Kuingia kwa mabao hilo kulionekana kuizindua Burundi na kuanza kuonyesha makucha yao kwa kufanya mashambulizi mengi katika lango la Tanzania na dakika ya 18 nusura Fabrise Nininahazwe aisawazishie timu yake baada ya kupiga shuti kali lakini likapanguliwa kiufundi na kipa Aishi Manuna na kuwa kona.
Jitihada za wachezaji wa Burundi zilizaa matunda baada ya kufanikiwa kusawazisha bao hilo katika dakika ya 25 lililofungwa na Ninihazwe,aliyemtoka beki wa kushoto wa Tanzania Miraji Adam na kufunga kirahisi.
Bao hilo lilionekana kuivuruga kabisa Tanzania iliyokuwa chini ya kocha Mart Nooij, na kuwaacha Burundi wakiutawala mchezo huo na Ninihazwe, aliyekuwa mwiba mchungu kwa mabeki wa Tanzania nusura aifungia bao la pili timu yake baada ya mpira wakichwa alioupiga dakika ya 32 kudakwa na Manula na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 1-1.
Kipindi cha pili Vijana wa kocha Rainer, walionekana kupania kuibuka na ushindi wa ugenini baada ya kuanza kwa kasi huku wakiutawala mchezo na kuliandama lango la Tanzania na kupoteza nafasi nyingi za mabao walizozipata .
Katika dakika ya 57 mshambuliaji wa Burundi Laudit Mavugo, alikosa bao la wazi akiwa amebaki yeye na kipa wa Tanzania lakini mpira wa kichwa alioupiga ulipanguliwa na kipa huyo na kuwa kona isiyokuwa na mazara.
Katika kipindi hicho cha pili kikosi cha Tanzania kilionekana kuzidiwa kabisa hasa eneo la kiungo na kuwaacha wapinzani wao Burundi wakicheza wanavyo taka kitu ambacho kilisababisha wapate bao la pili dakika ya 78 mfungaji akiwa Nassoro Niyunkuru alimalizia kwa shuti kali krosi ya Fiston Abdulrazak.
Pamoja na Tanzania kufanya mabadiliko kadhaa ya wachezaji kwa kumtoa Friday na kumuingiza Shiza Ramadhani, Omar Njenje lakini timu hiyo haikuweza kupata bao la kusawazisha.
Zikiwa zimesalia dakika 10 mpambano huo kumalizika Tanzania ilionekana kuzinduka na kufanya mashambuliaizi mengi kwenye lango la Burundi lakini wapinzani wao walijipanga vyema na kuondosha hatari zote langoni mwao.
Tanzania: Aishi Manula Adam Miraji,Gidael Michael,Jorome Mgeveke/Emmanuel SemwandaEndrew Vicent,Salim Mbonde,Rashind Yusufu/Omari Njenje,Hassan Banda,Atupele green, Klevin Friday/Abubakar Mohamed,Hussein Moshi.

No comments:

Post a Comment