


Phelan amesema: “Wameleta Watu wapya wenye mtazamo mpya na kumweka pembeni Tony Strudwick ambae ndie alikuwa Mkufunzi wa Mazoezi na aliemjua kila Mchezaji wa United nje ndani.”
Phelan, mwenye Miaka 52, ndie aliekuwa Meneja Msaidizi chini ya Sir Alex Ferguson kwa Miaka Mitano na hivi sasa ni Kocha wa Timu ya Kwanza huko Norwich City.

Kocha huyo amesema mtindo na mfumo mpya wa Mazoezi huenda ndio ulisababisha kina Michael Carrick, Phil Jones, Rafael na Radamel Falcao kuwa nje kwa kipindi kirefu wakiwa na maumivu.
Phelan ameeleza: “Kinachotokea ni Wachezaji wale wale kuumia kila mara na ni lazima utafute sababu. Nadhani ni tatizo la kubadili mfumo wa Mazoezi.”
No comments:
Post a Comment