Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 23, 2014

BRENDAN RODGERS AKERWA NA BALOTELLI KUBADILISHANA JEZI NA PEPE WAKATI WA MAPUMZIKO JANA.! WAKIAMBULIA KIPIGO CHA BAO 3-0 KUTOKA KWA REAL!


Kocha wa Liverpool Brendan Mario Balotelli sasa anakabiliwa na kisago toka kwa Meneja wake Brendan Rodgers kwa kubadilishana Jezi na Sentahafu wa Real Madrid Pepe wakati wa Haftaimu wa Mechi iliyochezwa Anfield Jumatano Usiku na Liverpool kutandikwa 3-0.

Akiteta na Pepe na baadae kupeana jeziMipango ya Jezi ilianzia hapa kwenye stori za hapa na pale wakitoka nje ya Uwanja kwenda kupumzikaNipe jezi!Wakati huo wa Mapumziko Liverpool ilikuwa tayari iko nyuma kwa hizo Bao 3-0 zilizofungwa na Cristiano Ronaldo na mbili za Karim Benzema huku Mario Balotelli akizunguka tu Uwanjani na kubadilishwa kabla Kipindi cha Pili kuanza na nafasi yake kuchukuliwa na Adam Lallana.
Akiongea kuhusu tukio hilo la Balotelli kubadilishana Jezi, Rodgers alisema: “Ni kitu ambacho sikikubali. Kama unataka kufanya hivyo, fanya mwisho wa Mechi. Nitalishughulikia suala hili Alhamisi.”
Msimu uliopita tukio kama hilo lilitokea huko Stamford Bridge Liverpool walipocheza na Chelsea na Beki wao Mamadou Sakho kubadilishana Jezi na aliekuwa Straika wa Chelsea Samuel Eto'o na kumuudhi Brendan Rodgers ambae Jana alilikumbushia na kusema walilishughulikia ndani ya Klabu. Mbali ya kugubikwa na tukio hili la kubadilishana Jezi, Balotelli hivi sasa anasakamwa kwa uchezaji duni huko Liverpool lakini Meneja Rodgers amesema Jana alimtoa wakati wa Haftaimu ili kubadili mbinu tu.
Brendan Rodgers ameeleza: “Ni mbinu tu. Nilidhani tunahitaji nguvu na wepesi zaidi kwenye Kiungo na nilitaka Mtu mwepesi kuwahangaisha Masentahafu wao na niliona Raheem Sterling anaweza hilo. Adam Lallana aliingia kuleta uhai kwenye Kiungo na alifanya bidii sana.”Karim Benzema akishangilia moja ya bao zake Aaaah!!

No comments:

Post a Comment