Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 23, 2014

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: LIVERPOOL 0 vs 3 REAL MADRID, CRISTIANO RONALDO AFUNGA BAO LA KWANZA ANFIELD!! KARIM BENZEMA AKIFUNGA MBILI!

3-0!!Wachezaji wa Real wakimpongeza mwenzao Karim Benzema baada ya kufunga bao la tatu kipindi cha kwanza cha dakika 45.
Hii ni mara ya kwanza kwa Real kuifunga Liverpool katika Mashindano ya Ulaya baada ya kufungwa Mechi zao zote 3 walizokutana huko nyuma na ni Cristiano Ronaldo ndie aliefungua milango kwa kutengeneza na yeye mwenyewe kupachika Bao la kifundi baada ya kucheza ‘moja mbili’ na James Rodriguez kwenye Dakika ya 23.Cristiano Ronaldo akishangilia bao lake la kwanza...
Bao la tatu lilifungwa na Karim Benzema tena baada ya kupigwa kona na Pepe kujitwisha kichwa kwenye eneo hatari ndani ya box na hatimae Karim Benzema kuupata na kuusindikiza langoni mwa Liverpool na kumfunga kipa Mignolet na kufanya 3-0 katika dakika ya 41.Karim Benzema akiruka juu na kufunga bao la pili.Cristiano Ronaldo akikatiza mbele..Cristiano Ronaldo aliipachikia bao la kwanza kipindi cha kkwanza dakika ya 23 baada ya kutengeneza pasi na kurudishiwa na James Rodríguez na kufunga bao hilo na kufanya 1-0 dhidi ya Wenyeji Liverpool. Bao la pili lilifungwa na Karim Benzema dakika ya 30 kwa kichwa baada ya kupokea Krosi safi kutoka kwa Toni Kroos.Mario Balloteli wakati wa mapumziko aliomba jezi kutoka kwa mchezaji Real.

No comments:

Post a Comment