Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, September 30, 2014

RATIBA - UEFA CHAMPIONS LEAGUE: LEO JUMANNE BARCELONA vs PSG, NEYMAR NA MESSI KUENDELEZA MAKALI YAO??


Paris St-Germain watatinga Mechi hii ya Nyumbani kwao ya Kundi F dhidi ya FC Barcelona bila ya Straika wao mahiri Zlatan Ibrahimovic ambae ameumia kifundo cha Mguu.
Katika Mechi za kwanza za Kundi lao, PSG ilitoka Sare na Ajax na Barcelona kuichapa Apoel Nicosia Bao 1-0.

Wakati PSG hawajafungwa hata Mechi moja katika Mechi 9 Msimu huu, ingawa 6 kati yake ni suluhu, Barcelona wamekuwa hatari mno huku Mastraika wao Messi na Neymar wakicheka na nyavu kila mara na Juzi waliibamiza Granada 6-0 huku Neymar akipiga Hetitriki na Messi Bao 2.

Mechi hii inawakutanisha Mameneja wa Timu hizi mbili, Laurent Blanc wa PSG na Luis Enrique wa Barca, ambao waliwahi kucheza pamoja wakiwa Barcelona katika Msimu wa 1996/97 na kuiwezesha kutwaa Kombe la Washindi wa Ulaya, Copa del Rey na Spanish Super Cup.



RATIBA MECHI ZA LEO JUMANNE
Mechi zote kuanza Saa 21:45

Jumanne Septemba 30
KUNDI E
19:00 CSKA Moscow vs Bayern Munich
Manchester City vs Roma

KUNDI F
APOEL Nicosia vs Ajax
Paris St-Germain vs Barcelona

KUNDI G
FC Schalke 04 vs NK Maribor
Sporting Lisbon vs Chelsea

KUNDI H
BATE Borisovs vs Athletic Bilbao
Shakhtar Donetsk vs FC Porto

No comments:

Post a Comment