
Katika Mechi za kwanza za Kundi lao, PSG ilitoka Sare na Ajax na Barcelona kuichapa Apoel Nicosia Bao 1-0.

Wakati PSG hawajafungwa hata Mechi moja katika Mechi 9 Msimu huu, ingawa 6 kati yake ni suluhu, Barcelona wamekuwa hatari mno huku Mastraika wao Messi na Neymar wakicheka na nyavu kila mara na Juzi waliibamiza Granada 6-0 huku Neymar akipiga Hetitriki na Messi Bao 2.

Mechi hii inawakutanisha Mameneja wa Timu hizi mbili, Laurent Blanc wa PSG na Luis Enrique wa Barca, ambao waliwahi kucheza pamoja wakiwa Barcelona katika Msimu wa 1996/97 na kuiwezesha kutwaa Kombe la Washindi wa Ulaya, Copa del Rey na Spanish Super Cup.
RATIBA MECHI ZA LEO JUMANNE
Mechi zote kuanza Saa 21:45
Jumanne Septemba 30
KUNDI E
19:00 CSKA Moscow vs Bayern Munich
Manchester City vs Roma
KUNDI F
APOEL Nicosia vs Ajax
Paris St-Germain vs Barcelona
KUNDI G
FC Schalke 04 vs NK Maribor
Sporting Lisbon vs Chelsea
KUNDI H
BATE Borisovs vs Athletic Bilbao
Shakhtar Donetsk vs FC Porto
No comments:
Post a Comment