Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, January 17, 2014

KOCHA SIMBA AOMBA UONGOZI UMTAFUTIE MECHI MBILI ZA KIRAFIKI

Kocha mkuu wa wekundu wa Msimbazi Simba Mcroatia Zdravko Logarusic ameuomba uongozi wa wekundu hao kumpatia michezo miwili zaidi ya maandalizi kabla ya kuingia katika mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara maarufu kama ligi kuu ya Vodacom.
Logarusic ameomba michezo hiyo ikiwa ni siku moja tu mara baada ya kurejea kutoka visiwani Zanzibar ambako Simba walikuwa wakishiriki michuano ya kuadhimisha miaka hamsini ya mapinduzi ya Zanzibar ambako Simba ilifanikiwa kufika fainali na kufungwa na KCC ya Uganda kwa bao 1-0.

Akiongea mara baada ya kuwasili jijini Dar es Salaam, kocha msaidizi wa wekundu hao Selemani Matola amesema bosi wake ameuomba uongozi kumtafutia michezo miwili ya maandalizi zaidi, huku mchezo mmoja ukiwa na timu ya nchini Tanzania na mchezo mwingine dhidi ya timu kutoka nje ya nchi.
Matola amesema kimsingi wamekubali matokeo ya mchezo wa fainali na kwamba wanatengeneza kikosi kwa ajili ya ligi hivyo basi michezo hiyo itawasaidia kurekebisha makosa yaliyojitokeza kwenye michuano ya kombe la mapinduzi.  

No comments:

Post a Comment