Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, January 17, 2014

COPA del REY: GETAFE CF 0 vs BARCELONA 2 (Agg 0-6) MESSI AIKUNG'UTA GETAFE BAO MBILI


Lionel Messi, ameifungia Timu yake Barcelona Bao 2 na kuihakikishia kucheza Robo Fainali ya Kombe la Mfalme wa Spain, Copa del Rey, baada baada kuibwaga Getafe Bao 2-0 na kuitupa nje.
Messi alipiga Bao zake kwenye Dakika za 44 na 63 na kuifanya Barca itinge Robo Fainali kwa Jumla ya Bao 6-0 baada kuitwanga Getafe 4-0 katika Mechi ya Kwanza.
Xavi aliingizwa Dakika ya 70 kumbadili Cesc Fabregas na hii ilikuwa Mechi yake ya 700 kwa Barcelona akizidi kupaa akiwa ndie Mchezaji alieichezea Klabu hiyo Mechi nyingi kupita yeyote.
Awali, Real Sociedad, ikicheza Ugenini, iliibwaga Villareal Bao 1-0 baada kutoka Sare 0-0 katika Mechi ya Kwannza.

Dani Alves kulia akichuana vikali na mchezaji wa Getafe midfielder Angel LafitaNeymar aliumia mguu jana wakati wanainyuka Getafe bao 2-0, na wenda akawa nje kwa mudaNeymar aliumia ankle kwenye msuguano akiwa na mchezaji wa Getafe Alexis Ruano.
COPA del REY
RATIBA
Robo Fainali
Mechi ya Kwanza Jan 21-23, Marudiano Jan 28-30
A -RCD Espanyol v Real Madrid
B -Levante v FC Barcelona
C -Real Sociedad v Real Racing Santander
D -Atlético de Madrid v Athletic de Bilbao
Nusu Fainali
Mechi ya Kwanza Feb 5-6, Marudiano Feb 12-13
Mshindi Mechi B v Mshindi Mechi C
Mshindi Mechi A v Mshindi Mechi D
Nusu Fainali
Mechi ya Kwanza Feb 5-6, Marudiano Feb 12-13
Fainali
Aprili 19

No comments:

Post a Comment