Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, September 30, 2013

WALIOPASWA KUMRITHI FERGIE BADALA YA MOYES


KITABU cha maisha ya Jose Mourinho, kimesema kuwa kocha huyo wa Chelsea, alimwaga machozi baada ya David Moyes, kupewa jukumu la kurithi mikoba ya Sir Alex Ferguson.
Mwishoni mwa wiki Manchester United walipata kipigo cha pili mfululizo katika Ligi Kuu England.
Kwa wale waliokuwa wakiamini kocha huyo wa zamani wa Everton, Moyes, atafanya vizuri mwishoni mwa msimu akiwa Old Trafford, wameanza kujiuliza kuhusiana na hali hiyo itachukua muda gani, baada ya Manchester Unite kupata kipigo cha pili mfululizo kwenye Ligi Kuu England, tena wakiwa nyumbani dhidi ya West Bromwich Albion.
Hivyo imeonyesha wazi kuwa Moyes, ameshindwa kuimudu timu, baada ya mwenyewe kukiri kuwa amerithi mikoba ya kocha mkubwa na matokeo mabaya huenda yakawandama zaidi.
Makocha watano ambao wangepaswa kumrithi Ferguson, badala ya Moyes ndani ya Old Trafford.
 
5- Carlo Ancelotti
Kocha Carlo Ancelotti, aliweka wazi kuwa ataondoka Paris Saint-Germain mwishoni mwa msimu uliopita na klabu pekee iliyoonyesha dalili ya kumnyemelea ilikuwa ni Real Madrid.
Ancelotti, ambaye ana historia nzuri ya kuongoza klabu kubwa, ingawa aliwahi kuinoa Chelsea, lakini upendo wake kwa Blues usingeweza kumfanya akatae ofa ya kuinoa klabu hiyo ya Old Trafford.
Ukiangalia jinsi alivyokuwa akifanya kazi AC Milan na PSG, alikuwa akijenga mawasiliano mazuri na wachezaji wenye majina makubwa, ambao angeweza kuwanasa kwa urahisi akiwa Manchester United.
 
4- Jurgen Klopp
Ni mtu ambaye alikuwa kwenye orodha ya makocha wanaowaniwa kumrithi Fergie, lakini hakuna mazungumzo yaliyofanyika.
Klopp, amejijengea jina kubwa kwenye soka kwa kupata mafanikio makubwa, baada ya kuwabadilisha chipukizi wa Borussia Dortmund na kuwa timu yenye uwezo wa kuleta ushindani na vikosi vikubwa.
Ni Mjerumani mwenye macho ya kugundua vipaji na kuvitumia uwanjani, jambo ambalo limeweza kumpa heshima Ulaya na itashangaza kama hakuna klabu hata moja kubwa ambayo itakayojaribu kumnasa.
United walikuwa na nafasi hiyo ya kumpa mikoba ya Fergie kocha huyo, ili apate changamoto za Ligi Kuu England, lakini wenyewe waliamua kumpa jukumu hilo Moyes.
Uhusiano wa Klopp na wachezaji, lazima wachezaji kadhaa wangemfuta kocha hyo England.
 
3- Laurent Blanc
Blanc alikuwa United kama mchezaji na sasa amepewa jukumu la kumrithi Carlo Ancelotti katika klabu ya Paris Saint-Germain, hivyo angekuwa mtu sasa kutua Old Trafford.
Kocha huyo wa Ufaransa, alifanya kazi nzuri alipokabidhiwa kikosi cha Bordeaux na angeweza kupewa jukumu la kuinoa United.
Blanc, mwenye umri mdogo wa kuweza kuingoza klabu hiyo ya Old Trafford kwa muda mrefu, huku akiwa uwezo wa kuiongoza timu kwenye hali yoyote.
 
2- Pep Guardiola
Wakati Moyes anapewa jukumu la kuinoa United, tayari Pep Guardiola alikuwa ameshamwaga wino kwenye klabu ya Bayern Munich.
Lakini, kama United wangefikiria kumfuata mapema ili aweze kumrithi Sir Alex, wangeweza kumshawishi na Ligi Kuu England ndio alikuwa akiitaka, ili kujijengea heshima.
Kocha huyo mwenye malengo, alifanikiwa  kuifanya klabu ya Barcelona iliyokuwa na vipaji na kuifanya iweke historia kubwa kwenye soka.
 
1- Jose Mourinho
Huenda Mourinho amelia au hakulia kwa kuchaguliwa Moyes badala yake, lakini  kuinoa United ni kibarua alichokuwa akikitaka kwa muda mrefu.
Special One ni kocha ambaye anapenda mambo yaende anavyotaka yeye na ana njia zake, lakini jambo la kufurahisha ni kwamba anakuwa na uhakika wa mafanikio na mataji.
United walipashwa kumpa kumpa kocha huyo wa Ureno kibarua hicho.
Aba uzoefu wa kunyakua mataji kwenye ligi mbalimbali duniani, ikiwemo Ligi Kuu England, Serie A, La Liga na Ureno.
Klabu hiyo ya Old Trafford kama ingemchukua Mourinho, ungekuwa ni uamuzi sahihi wa kumrithi Ferguson.

No comments:

Post a Comment