![](http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/01399/mancity_1399048c.jpg)
MANCHESTER, England
NAHODHA wa Manchester
City, Vincent Kompany, ametoboa siri
iliyoifanya timu yao ikaibuka na ushindi mnono
wa mabao 4-1 katika mechi ya Ligi Kuu ya England dhidi ya mahasimu wao,
Manchester United, akidai ni kujituma kwao.
Anasema, timu nzima ilijituma siku hiyo kwa vile kila mmoja
aliuona ushindi kwa City ulikuwa muhimu na wenye maana zaidi kuliko ilivyokuwa
kwa United.
Ni kweli, kujituma huko kulionekana kulipa na kama
wasingefanya hivyo, wasingeweza kushinda mechi yao. Lakini kwa wale walioitazama mechi hiyo
vizuri, watakiri kwamba
City, inayonolewa na
kocha Manuel Pellegrini pia iliizidi Man United kwa kila idara uwanjani.
United ilionekana kupwaya kwa sababu ilikuwa na pengo kwenye
safu yake ya ushambuliaji, kutokana na kutokuwepo kwa Robin Van Persie. Hata
hivyo hiyo inaweza isiwe sababu kwani Man City
ya Jumapili, ilikuwa sawa sawa.
Kabla ya mechi hiyo, City ya Pellegrini, haikuwa imewahi
kuonyesha uzuri wowote na hakuna mtu ambaye angetegemea matokeo kama hayo, lakini kwa uchezaji ule, ilionekana kuwa ni
timu iliyojipanga vizuri zaidi kushinda vigogo wote msimu huu.
Nahodha wake, Vincent Kompany na kiungo Yaya Toure
walionekana kuwa wao ndio nyota wa mchezo kwa siku hiyo, baada ya kutawala safu
ya ulinzi na dimba la kati kiasi cha kuwadhibiti kabisa United.
Kompany alimficha kabisa, Wayne Rooney kwa zaidi ya dakika
60, wakati Toure alikuwa kinara katika kupandisha mashambulizi yote ya City
katikati ya dimba na kuifanya Man United kupoteana mara kwa mara.
Kiukweli, vita katika idara ya katikati ilikuwa kubwa
lakini, Toure alionekana kuimudu vilivyo.
Toure amekuwa akitumiwa na Pellegrini kama
kiungo mkabaji na kwa waliomuona siku hiyo watakubali uwezo wake. Alikuwa
akizuia mashambulizi yote yasifike kwao na akatawala kwa kuudhibiti mpira
usiende kwa maadui huku akipanda kuongeza nguvu.
Alifanya hivyo kwa dakika zote tisini, na matunda yake ya
kupanda mbele yalionekana baada ya kwenda kufunga bao moja kati ya manne.
Uhuru wake wa kupanda na kushuka huku akisaidiana na
Fernandinho, uliwafanya waonekane wameitimiza kazi yao ipasavyo, huku wakiwazidi Marouane
Fellaini na Michael Carrick.
Pellegrini anaitaka timu yake icheze kwa kumiliki mpira muda
mrefu na kwa kumtumia Toure, wamepata mchezaji sahihi wa kuwasaidia.
Alipiga pasi nyingi kuliko mchezaji yeyote wa timu yake,
ambapo idadi inaonyesha kuwa aliwazidi kwa pasi 52 sahihi katika mchezo mzima
na hadi hivi sasa anaongoza kwa wachezaji wote wa Ligi Kuu ya England.
Kabla ya mechi, ilidhaniwa kuwa winga wa City, Jesus Navas,
angeweza kuwa 'sumu' dhidi ya beki wa kushoto wa United, Patrice Evra, ambaye
alifikiriwa kuwa ndiye angekuwa mwiba wa kuanzisha mashambulizi.
Vile vile wengi walitarajia kuwa winga wa United, Antonio
Valencia angeweza kuwa hatari kwa wapinzani wao hao kutokana na kucheza upande
wa beki, Aleksandar Kolarov, ambaye hakabi sana.
Ukweli ukawa kwamba, katika upande huo, Valencia
alifunikwa na badala yake Kolarov ndiye aliyeonekana kung'ara zaidi. Uchezaji
wa pasi za haraka wa City ulikuwa hatari kwa Man United pande za pembeni,
ambapo mabeki walikuwa wakipanda na kushuka muda wote, Kolarov akiongoza.
Bao la kwanza la City, lilikuwa ni mfano mzuri wa aina hiyo
ya uchezaji.
Navas aliiba mpira na kuurudisha kwa kipa wake, Joe Hart.
Baada ya kipa huyo kuondoa hatari, ulikwenda moja kwa moja kupigwa kichwa na
Rio Ferdinand na kunaswa na Samir Nasri.
Nasri aliuchukua haraka na kumpasia Kolarov ambaye alikuwa
akipanda kwa kasi, huku Valencia
akishindwa kumkaba. Valencia
alionekana mvivu kupita kiasi, pengine kutokana na kuzidiwa na akamuachia kazi
Chris Smalling ya kuwadhibiti watu wawili, jambo ambalo hakuliweza na
kusababisha kufungwa bao.
Sehemu nyingine ya sababu ni kwamba, Toure hakuwa na kazi
kubwa ya kupasua katikati na hakuwa na hofu yoyote ya kuzuiwa na watu kama
Fellaini au Carrick, hata kama wote wawili
wangemfukuza nyuma yake.
Fellaini na Carrick walikuwa wakichunga zaidi pindi Toure
alipokuwa akiwafuata na wakasahau kwamba walikuwa wanaachia mwanya kwa
wachezaji wengine kuidhuru timu yao.
Haikutarajiwa kama Carrick angeweza kupanda mbele na hata
Fellaini alipojaribu kufanya hivyo hakuweza kuleta madhara yoyote zaidi ya kile
alichokifanya dakika ya 53 tu.
Toure na Fernandinho walimudu kucheza kama viungo huru, kwa
sababu timu yao ilijipanga sawasawa katika idara hiyo na walikuwa na watu wa
kazi upande wa ushambuliaji, kotekote kuanzia upande wa pembeni au katikati.
United haikufanya shambulizi lolote kutokea pembeni hadi City
ilipokuwa mbele kwa mabao 4-0, ndipo waliposhtuka.
Katika dakika zote 45 za kipindi cha kwanza, Fellaini alionekana
kujaribu kukaba tu, Danny Welbeck akawa kama
mtoto yatima mbele peke yake na United haikuweza kuwa na madhara yoyote.
Ni kama vile Man United haikujua ni kwanini imeamua kumnunua
mtu kama Fellaini na kumchezesha nafasi ya
ukabaji wakati anapaswa kuwa kwenye nafasi ya ushambuliaji.
Katika mechi hiyo, United walipaswa kumtumia mbele badala ya
ukabaji ili asaidie kupeleka mashambulizi kwa timu pinzani na hilo alilidhihirisha kipindi cha pili (dakika
ya 68), alipoweza kupanda mbele na kumpa kipa wa City, Hart usumbufu wa kuokoa
hatari yake ya kwanza kubwa.
Baada ya mechi kumalizika, takwimu zinaonyesha kuwa alikuwa
miongoni mwa wachezaji waliomudu kugusa mpira mara nyingi zaidi hata alipohamia
mbele kwenye eneo la wapinzani.
Lakini kwa upande wa ukabaji, alionekana kupotea na
kushindwa kugusa baadhi ya mipira iliyokuwa ikiingia kwenye eneo lao na
alifanya kosa la kumpoteza, Toure kwenye kona na kusababisha wafungwe bao la
pili.
Pia analazimika kubeba lawama kwa kushindwa kuwasiliana na
wenzake na kumruhusu, Sergio Aguero kumtoka na kufunga bao la tatu.
Uchezaji wa Rooney siku hiyo ulionekana kumkuna kocha wake,
David Moyes ambaye alimsifia lakini, kwa kipindi hiki ambacho, Van Persie
amekosa mechi yake ya kwanza ya Ligi Kuu ya England tangu atue Old Trafford mwaka
2011, tunaweza kuona ni jinsi gani Mholanzi huyo ana umuhimu kwenye kikosi cha
Mashetani hao Wekundu.
Ni sawa na alivyo Kompany kwa upande wa Man City;
haiwezi kuwa nzuri bila ya yeye kuwepo katika safu ya ulinzi.
Lakini swali ambalo mashabiki wanaweza kuendelea kujiuliza
kuhusu Man United baada ya mechi chache za mwanzo msimu huu ni kwamba je,
baadhi ya wachezaji wake wana uzuri kama
unaofikiriwa? Kama mwedo wao utaendelea hivyo,
hatutegemei iwapo timu hiyo itatwaa ubingwa.
Mabadiliko ambayo Moyes aliyafanya wakati timu yake ikiwa
nyuma kwa mabao 4-0 kumuingiza Tom Cleverley badala ya Ashley Young,
ilidhihirisha ni jinsi gani ina uhaba wa viungo wa ukweli kuweza kukabiliana na
timu ngumu.
@ Ingekuwa vipi Ligi Kuu England bila ya Wenger?
LEO
Jumatatu kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, anafikisha miaka 17 ndani ya klabu
hiyo ya Emirates.
Lakini
mwishoni mwa wiki alisheherekea kufikisha miaka hiyo 17, tangu atue kwenye
klabu hiyo mwaka 1996 kwa kuichapa Swanasea
City mabao 2-1.
Mchezaji
wa zamani wa Liverpool, Jamie Carragher,
ambaye ni mchambuzi wa mtandao wa Daily Mail, aliandika kuhusiana na Wenger
akisema: “Wote tunapaswa kuwa mashabiki wa Arsenal.”
Mawazo
hayo hayawezi kukubaliwa na mashabiki wa
White Hart Lane wala wale wa Stamford
Bridge, Manchester hata wa Merseyside. Lakini msimu
huu wote tunapaswa tuwe mashabiki wa Arsenal, aliandika Carragher.
Aliendelea
kusema kuwa kama Arsenal watafanikiwa, basi hiyo ina maanisha Wenger atabaki
Ligi Kuu England
na ukweli ni kwamba anahitajika kubaki.
Filosofia
ya Wenger imeleta mambo makubwa katika soka la England
na soka lingekuwa bofu kama sio yeye.
Ligi ya England isingekuwaje kama kama
sio Wenger? Klabu zisingefikiria kutafuta makocha wakigeni kwa haraka kama asingefanya lolote.
Mafanikio
yake yamefungua milango kwa makocha wengine kutua England, tangu kuwasili kwake
Arsenal mwaka 1996, makocha 47 kutoka
sehemu wameajiriwa kwenye klabu kubwa, ukilinganisha na makocha 120 wa England.
Hiyo ni idadi ya ajabu.
Hakuna
ubishi kwamba bila ya Wenger, kusingekuwepo na Jose Mourinho, Rafa Benitez,
Roberto Mancini au Carlo Ancelotti.
Bila ya
Wenger, isingewezekana kumuona Thierry Henry, Cesc Fabregas na Robert Pires na
wachezaji wengine wengi kutoka nje, ambao wameweza kubadilisha soka la England.
Beki huyo
wa Reds, alisema kuwa Wenger, ndiye aliyemtia hofu na kumfanya aongeze kiwango
chake cha soka, wakati huyo akicheza mpira kabla ya kustaafu.
Arsenal
alifanikiwa kutwaa mataji mbalimbali
kutoka mwaka 2002-2004, ambapo kikosi chake kilifanikiwa kuitwa kikosi
kilisichofungika, baada ya kumaliza msimu bila ya kufungwa hata mechi moja.
Wachezaji
wenye kiwango kizuri na wenye uwezo wa kukimbia — walikuwa na kila kitu. Hata
wachezaji wa upinzi waliposimama nao kwenye vyumba vya kubadilishia nguo,
walianza kuogopa kabla ya mechi.
Walikuwa
wachezaji wazuri na kuwa na timu ambayo ilikuwa ya kiufundi na nguvu kidogo.
Ilikuwa ni timu ambayo imeungana pamoja kuanzia mlinda mlango hadi
washambuliaji.
Wachezaji
walikuwa wamejengeka kimwili na kama utajaribu
kuwasukuma unaweza kuanguka mwenyewe.
Ikiwa
unacheza beki wa kulia kwa timu pinzani, halafu ukakutana na Arsenal ya wakati
huo, utakuwa na kazi ngumu, kutokana na kuwepo na wachezaji kama
Henry, Ashley Cole na Pires.
Wachezaji
hao walikuwa na uwezo wa kukufanya kitu kibaya kutokana na uwezo wao wa
kukokota mpira kwa kazi na kumfanya beki
akose muda wa kufikiria cha kufanya.
Heshima
ya Wenger ilikuwa juu, akiwa ameshinda taji la Ligi Kuu England, mataji
mawili ya Kombe la FA na mengine mawili ya Ngao ya Jamii katika muda wa misimu
mitatu.
Lakini
kwa sasa anaweza kuonekana kituko kwa watu kwa kushindwa kunyakua hata taji
moja katika miaka tisa.
Arsenal
wameshindwa kushindana na Manchester
City na Chelsea, kutokana
na matumizi mabaya ya fedha, huku wengine wakiiga mfumo wa Wenger kununua
chipukizi kutokana nje.
Ijumaa
iliyopita kulikuwa na kauli ya kumuunga mkono kocha huyo, kutoka kwa tajiri
mwenye hisa nyingi kwenye klabu hiyo, Stan Kroenke.
Lakini,
huu si wakati wa kuanza kumsifia Wenger, bali mashabiki na wadau wanapaswa
kusubiri hadi majira ya Krismasi. Kwa sasa ni mapema sana
kusema kitu kwa Arsenal, ingawa wanaongoza Ligi Kuu England.
Bila ya
shaka wana mambo mengi ya kuwathibitishia na wana kikosi cha ukweli kuweza
kuvaana na Manchester
City, Manchester United
na Chelsea.
Ushindi mmoja
walioupata dhidi ya mahasimu wao Tottenham, kikosi pekee chenye upinzani ambacho Arsenal wamekutanana nacho,
hautoshi kuwapima Gunners.
Wakiwa
chini ya Wenger, wamefanikiwa kufuzu kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa
muda wote wa miaka 16, lakini wameshindwa kunyakua Kombe la FA ama la ligi,
pamoja na kuwepo ‘top four’, kutokana na kutokuwa wazuri.
Wengi wa
mashabiki wanaweza kuwa wamechoshwa na Wenger kwa kuwa wanaijua klabu yao, lakini mara nyingi
wale ambao wamekuwa wakimkasirikia pale timu inapovurunda ila ikifanya vizuri
wamekuwa wakigeuka na kucheka baada ya kuona mazuri.
Mwanzoni
mwa msimu, baada ya Arsenal kuchaowa mabao 3-1 dhidi ya Aston Villa, mashabiki
wengi walianza kumzodoa kocha huyo. Wengi wakisema hakuna jipya, wanaonekana
kuwa wadhaifu.
Lakini,
kuwasili kwa Mesut Ozil, kumewasaidia kufanya vizuri na kuongeza nguvu kwenye
kikosi hicho.
Ozil ni
mchezaji pekee mwenye kiwango kizuri, ambaye amewasili Arsenal siku kabla ya
dirisha la usajili kufungwa na kuifanya timu hiyo kuwa ya kuvutia katika wiki
za mwanzoni, lakini mambo yanaweza yakawa magumu wiki hii kwa kukutana na Napoli hapo kesho.
Lakini
kuna maeneo muhimu ambayo yanatakiwa yawekwe vizuri kwenye kikosi hicho.
Watakuwa kwenye matatizo kama mshambuliaji wao Olivier Giroud atapata majeruhi,
lakini pia wanapaswa watoe ofa kwa ajili ya mlinda mlango wa Real Madrid, Iker Casillas au Victor Valdes wa Barcelona kwa ajili ya
kuwasajili Januari mwakani, ili wawe na mlinda mlango mwenye kiwango
wanaemhitaji.
Wanaweza
wakamaliza wakiwa ‘top four’ tena. Lakini tumtarajie kumuona Wenger kuingia
sokoni dirisha la usajili la January na kusajili wachezaji wengine wenye
kiwango, ili waweze kupambana na kuweza kuwania taji.
Carrangha,
alimaliza kwa kusema kuwa tunamtaka abaki, ili tupata kuona soka zuri zaidi la
Arsenal na wachezaji atakaowazalisha.
Tunapaswa
kuwaunga mkono Arsenal msimu huu. Wenger anahitaji kipindi kingine cha kunyakua
mataji na wote tunapaswa kumtakia mafanikio mema, ili soka la England lipate
kufanikiwa kutoka kwake.
Miaka ya Wenger, Arsenal
1996-97: Nafasi ya tatu Ligi Kuu England
1997-98:
Mabingwa wa li, Kombe la FA
1998-99:
Mshindi wa pili wa ligi
1999-00:
Mshindi wa pili wa Kombe Uefa na mshindi wa pili Ligi Kuu England
2000-01:
Mshindi wa pili wa ligi na Kombe la FA
2001-02:
Mabingwa wa li na Kombe la FA
2002-03:
Kombe la FA na washindi wa pili wa ligi
2003-04:
Mabingwa wa ligi
2004-05:
Washindi wa pili wa ligi na Kombe la FA
2005-06:
Washindi wa pili wa ligi
2006-07:
Nafasi ya nne ya ligi na nafasi ya pili wa Kombe la Ligi
2007-08:
Nafasi ya tatu Ligi Kuu England
2008-09:
Nafasi ya nne Ligi Kuu England
2009-10:
Nafasi ya tatu Ligi Kuu England
2010-11:
Nafasi ya nne Ligi Kuu England,
washindi wa pili wa Kombe la Ligi
2011-12:
Nafasi ya tatu Ligi Kuu England
2012-13:
Nafasi ya nne Ligi Kuu England
No comments:
Post a Comment