Mechi
za nyumbani za timu ya Kanembwa JKT ya Kigoma iliyoko Ligi Daraja la
Kwanza (FDL) sasa zitachezwa katika Uwanja wa Kawawa badala ya ule wa
Lake Tanganyika.
Uamuzi
wa kuhamishia mechi hizo Uwanja wa Kawawa ulioko Ujiji umetokana na
Uwanja wa Lake Tanganyika kutumiwa na Serikali katika Operesheni Ondoa
Wahamiaji Haramu inayoendelea nchini kwa sasa. Uwanja huo hivi sasa
unatumika kuhifadhi wahamiaji hao.
Kanembwa JKT inaanzia nyumbani kwa kuikaribisha Polisi Tabora. Mechi hiyo itachezwa Jumamosi (Septemba 14 mwaka huu).
No comments:
Post a Comment