Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, September 30, 2013

KIKOSI CHA MAN UNITED CHAMTIA HOFU MOYES, MOURIHNO ALIA NA VERTONGHEN NA ARSENAL, LIVERPOOL ZAMNYATIA BALOTELLI



MANCHESTER, England
KOCHA wa Manchester United, David Moyes ameshikwa na ‘kitete’ juu ya ubora wa kikosi chake baada ya timu hiyo kupigwa mabao 2-1 na West Bromwich Albion, Old Trafford kwenye mchezo wa Ligi Kuu England, juzi.
Man United imeweka rekodi mbaya zaidi ya mwanzo wa ligi katika kipindi cha miaka 24, kikosi cha Moyes kimefungwa mechi tatu kati ya sita na kufanikiwa kupata pointi saba tu mpaka sasa na hii ni rekodi mbovu zaidi ya United tangu msimu wa 1989-90, zama za mwanzo za Sir Alex Ferguson.
Moyes ameonyesha kuwa na hofu ya kushindwa kufanya vizuri kwenye michuano ya Klabu Bingwa Ulaya, kutokana na kikosi chake kukosa wachezaji wa kiwango cha dunia wa kutosha.
“Kushinda Ligi ya Mabingwa Ulaya, unahitaji wachezaji watano au sita wa kiwango cha dunia,” alisema Moyes.
“Angalia Bayern Munich, wanajaa. Angalia Barcelona, walikuwa nao siku za nyuma na Real Madrid, ambao wanaweza kuwa nao sasa. Hivyo ndivyo unatakiwa kuwa kama unataka kuchukua taji la Ulaya. Hatuna hilo bado, lakini tumejaza uzoefu.

“Nilipopewa kazi hii, ilikuwa lazima mabadiliko yafanyike na tukomae kadri siku zinavyozidi kusonga mbele.”
Moyes amekuwa na wiki ngumu baada ya Man United kufungwa mechi mbili mfululizo za Ligi Kuu England na Manchester City na West Brom na kocha huyo wa United amekiri kwamba matokeo ya timu hiyo yanamtisha, hasa kutokana na timu hiyo kushindwa kufunga mabao ya ‘muvu’ kwenye ligi tangu baada ya mechi ya Swansea.

“Yalikuwa matokeo mabovu na kiwango kibovu,” alisema Moyes, “Hatukuonyesha mchezo mzuri. Tulimiliki mpira sana kipindi cha kwanza, lakini nafasi hatukutengeneza. Na tulipozitengeneza hatukuzitumia. Walikuwa hatari zaidi kwenye mashambulizi ya kushtukiza katika kipindi cha kwanza na zaidi walitisha kipindi cha pili.
“Ndio ninahofu baada ya matokeo ya leo, lakini kwa sababu tu hatukucheza vizuri. Kuna mechi nyingi zinakuja, nitajaribu na kuweka mambo sawa kwenye mechi zijazo.”

Moyes aliongeza kwamba, kinachowaangusha ni kushindwa kutengeneza mabao ya muvu na siyo kwamba hawana washambuliaji au wameshindwa kuonyesha kiwango, anaamini kwamba wanahitaji kujituma zaidi.
Mskochi huyo alisema kwamba, kwenye mechi dhidi ya West Brom, wachezaji walikuwa hawana hamasa uwanjani na walistahili kufungwa kutokana na hilo.
United juzi ililala kwa mabao ya Morgan Amalfitano na Saido Berahino, huku bao pekee la Man United likifungwa na Wayne Rooney kwa njia ya adhabu.
@@@@
 
Mourinho alia na Vertonghen
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amemuangushia zigo la lawama beki wa Tottenham Hotspur, Jan Vertonghen kwa kumtafutia kadi nyekundu straika wake, Fernando Torres.
Katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, Mourinho anaamini kwamba, Vertonghen alimdanganya mwamuzi na kumtafutia Torres kadi ya pili ya njano na kusababisha straika huyo atolewe kwa kadi nyekundu.
“Timu yangu ilikuwa vizuri sana, mpaka mwamuzi alipofanya makosa, makosa makubwa ambayo yalichangia sana kusababisha matokeo yawe vile. Mwamuzi hana hatia, Mchezaji (Vertonghen) ndiye mwenye hatia. Alijidanganyisha kana kwamba ameguswa sana na Fernando (Torres) na mwamuzi akamuamini na kutoa kadi,” alisema Mourinho.
Mourinho anaamini kadi hiyo ya Torres aliyoipata zikiwa zimesalia dakika 10 mechi kuisha, kwa kiasi kikubwa iliinyima ushindi timu yake, ambayo ilikuwa ikishambulia kwa kasi wakati huo.
@@@@

  
Arsenal, Liverpool zamnyatia Balotelli
LONDON, England
ARSENAL na Liverpool zinaangalia uwezekano wa kumsajili straika mtukutu wa AC Milan, Mario Balotelli wakati wa dirisha dogo la usajili la Januari.
Kumekuwa na taarifa nchini Italia kwamba, Balotelli ‘Mad Mario’ tangu alipoondoka Manchester City amekuwa na vipindi tofauti akiwa AC Milan.
Pia amekuwa akikutana na tatizo la ubaguzi wa rangi kila kukicha kwenye majukwaa ya soka ya Italia, hivyo wachambuzi wa mambo wameanza kuamini kwamba kunauwezekano wa straika huyo kuuzwa kwa dau la pauni milioni 12 na Arsenal na Liverpool zinaweza kumtupia ndoano.

No comments:

Post a Comment