Hong
Kong, China
MABINGWA wa Ligi
Kuu England, Manchester United leo walifuta mzimu wa kufanya vibaya ziara yao
ya Mashariki ya Mbali baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya klabu
ya Kitchee ya Hong Kong.
Mabao ya vijana wa
David Moyes kwenye pambano hilo yaliwekwa kimiani na straika wake Danny
Wellbeck katika dakika 16 ya mchezo baada ya kazi nzuri iliyofanywa na winga wa
timu hiyo, Ashley Young.
Ikishambulia kwa
kasi, Man United ilipata bao la pili kupitia kwa beki wake Chris Smalling
katika dakika 22 baada ya kuunganisha wavuni krosi iliyopigwa na Tom Cleverley,
kabla ya Fabio da Silva kupachika bao la tatu hivyo kumaliza kipindi cha kwanza
ikiongoza kwa mabao 3-0.
Man United
ilikianza kipindi cha pili kwa kasi, ambapo shambulizi lake la kwanza lilizua
bao katika dakika ya 47 mfungaji akiwa
kiungo chipukizi Adnan Januzaj, kabla ya Lingard kupachika bao la tano.
Wenyeji walipata
mabao yao kupitia kwa Lam Kai Wai katika dakika ya 53 na Alex Alkande katika
dakika ya 69, katika mchezo huo ambao awali Man United walitaka kugoma kucheza
kutokana na ubovu wa sehemu ya kuchezea ya uwanja uliotumika.
Matokeo ya Man
United kabla ya mechi ya Jana, walipigwa 1-0 na Singha All Stars, wakashinda
5-1 dhidi ya A-League All Stars, wakapigwa 3-2 na Yokohama F-Marinos, kabla ya
kutoa sare ya 22 na Cerezo Osaka katika mechi yake ya mwisho.
No comments:
Post a Comment