Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 1, 2013

CAZORLA, NACHO WATEMWA ARSENAL

London, England

SANTI CAZORLA na Nacho Monreal watakosa safari ya Arsenal kwenda kujiandaa na msimu mpya mashariki ya mbali, jambo litakalowafanya kuhaha kupata namba katika kikosi cha kwanza mwanzoni mwa msimu.

Wahispania hao wemepewa muda zaidi wa kupumzika na Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger kutokana na kuwa katika michuano ya Kombe la Mabara iliyomalizika jana nchini Brazil, kwa timu yao kucheza fainali na wenyeji hao.

Wachezaji wengine wa Arsenal waliripoti mazoezini tangu Alhamisi kabla ya wiki hii kusafiri kwenda barani Asia kwa mechi nne za kirafiki.

Lakini Cazorla na Monreal hawatajiunga na wenzake hadi mwanzoni mwa Agosti. Katika michuano hiyo, Cazorla alicheza mechi dhidi Uruguay na Tahiti, wakati ambapo Monreal alionekana mara moja tu wakati Hispania ilipoibugiza Tahiti 10-0.

Baada ya safari hiyo ya Asia, Agosti 3 na 4, mwaka huu Arsenal itacheza dhidi ya Napoli na Galatasaray, mechi ambazo zitakuwa ni mapema mno kwa Cazorla na Monreal kucheza.

Bado itakuwa ni vigumu kwao kukubalika kucheza mechi ya ufunguzi ya Ligi Kuu England dhidi ya Aston Villa, Agosti 17.

No comments:

Post a Comment