Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

UNITED YAMFUNGA DE GEA KUTUA BARCELONA

Manchester, England

DAVID DE GEA yupo mbioni kuongezewa mshahara wake, ikiwa ni sehemu ya kumpongeza kwa kuonyesha kiwango bora na Manchester United msimu uliopita.

Kipa huyo wa Kimataifa wa Hispania, ana mkataba na Man United hadi 2016, lakini si miongoni mwa wachezaji wanaolipwa vizuri zaidi Old Trafford, kutokana na kitita chake cha pauni 55,000 anazopokea kwa wiki.

Lakini uongozi wa juu wa United, unatarajia kukaa chini na wawakilishi wa kipa huyo, 22, majira haya ya joto na kujadili uwezekano wa kupandisha maslahi yake hadi kufikia pauni 75,000 kwa wiki, ambazo wanaamini zitazima ndoto zake za kutaka kuhamia Barcelona.

Mhispania huyo ambaye ndiye kwanza amekiwezesha Kikosi cha Hispania U-21 kutwaa ubingwa wa Ulaya, alikuwa akihusishwa na Barca kwenda kurithi mikoba ya Victor Valdes, kabla ya kipa huyo kuamua kuitumikia kwa mwaka mmoja zaidi.


De Gea ambaye aliigharimu United pauni milioni 17.8 akitokea Atletico Madrid miaka miwili iliyopita, huduma yake bado inatamaniwa na wakali hao wa Nou Camp, lakini United ipo makini ikitambua kwamba atapewa nafasi kubwa wakati Valdes atakapoamua kuondoka.

No comments:

Post a Comment