Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 1, 2013

CHELSEA YAMALIZANA NA CAVANI

London, England

MSHAMBULIAJI wa Napoli, Edinson Cavani amemalizana na Chelsea, baada ya kukubaliana maslahi yake binafsi ya kujiunga na klabu hiyo majira haya ya joto.

Vyombo vya habari nchini Italia, vimeeleza kuwa Cavani amekubali kulipwa mshahara kiasi cha pauni milioni 7.2 kwa mwaka, lakini sasa itambidi kuishawishi Napoli kushusha ada yake ya uhamisho ili zoezi hilo likamilike.

Chelsea haipo tayari kulipa euro milioni 63 ambazo ni sawa na pauni milioni 53 zinazohitajika na Napoli, ili kuvunja mkataba wake, hivyo Cavani itabidi amshawishi Rais wa klabu hiyo, Aurelio de Laurentiis kushusha dau hilo.


Napoli inataka kumtwaa Ramires pamoja na fedha kama sehemu ya kukubali kumwachia Cavani, lakini Chelsea haipo tayari kuachana na Mbrazil huyo.

No comments:

Post a Comment