Redds Miss Sinza ambaye pia ni Redds Miss Tanzania, Brigitte Alfred alisisitiza jambo kwa warembo wa Redds Miss Sinza 2013 alipotembelea kambi ya mazoezi hiyo. Warembo hao watapanda jukwaani Ijumaa kuwania taji la mwaka huu. (Picha/Mpiga picha wetu).
Na Mwandishi Wetu
BENDI yenye chati ya juu kabisa katika muziki wa dansi nchini, The African Stars’ Wana Twanga Pepeta’ itaburudisha mashindano ya Redds Miss Sinza yaliyopangwa kufanyika Ijumaa (Juni 7) kwenye ukumbi wa Meeda Club wa Sinza jijini.
Majuto alisema kuwa Twanga Pepeta itakuwa ikitumbuiza kwa mara ya kwanza tokea mwaka jana mwezi julai ambapo ilitumbuiza katika mashindani hayo hayo ya kumsaka mrembo wa Sinza. Alisema kuwa hii ni faraja kubwa kwa mashabiki wa muziki wa dansi na wa masuala ya urembo kwani Twanga Pepeta itakuwa ikimvua taji Redds Miss Tanzania, Brigitte Alfred ambaye atakuwa anavua taji lake la kwanza.
Alisema kuwa jumla ya warembo 12 wamejitokeza kuwania taji la mwaka huu la Sinza nan i matarajio ya waandaaji kuwa Miss Sinza wa mwaka huu atatwaa taji hilo na kufuata nyayo za Brigitte ambaye aliweza kutwaa taji la Miss Kinondoni na baadaye Miss Tanzania.
“Tuna warembo bora ambao wamedhamilia kufanya kweli katika mashindano ya urembo mwaka huu, wamepania kulinda hadhi ya mwaka jana, hivyo mashabiki waje kuona warembo bora waliopania kufanya kweli katika mashindano hayo,” alisema.
No comments:
Post a Comment