Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

JE, VAN PERSIE ATAJUTA KUONDOKA ARSENAL?

Gonzalo Higuain: Argentina international backed to emulate Robin van Persie
MANCHESTER, England
UHAMISHO wa Robin van Persie kutoka Arsenal kwenda Manchester United, ndio uliotawala vichwa vya habari msimu uliopita.

Baada ya miaka nane akiwa London Kaskazini chini ya Arsene Wenger, Mholanzi huyo aliamua kukataa kusaini mkataba mpya na hivyo kuuzwa Man United kwa pauni milioni 24.5.
Alikuwa ameshinda tuzo ya ufungaji bora kwenye msimu wake wa mwisho akiwa na The Gunners na kushinda tena kiatu cha dhahabu msimu uliopita akiwa na Red Devils, baada ya kufunga mabao 26 kwenye mechi 38 alizocheza.

Lakini mwisho wa msimu uliopita, Sir Alex Ferguson alitangaza kustaafu kufundisha soka baada ya miaka 26 akiwa na Manchester United. Fergie alikuwa gundi iliyoiunganisha timu pamoja na bila shaka kocha bora wa muda wote wa Uingereza.
Upande wa pili, msimu wa 2011-12 ulikuwa msimu mwingine mbovu Emirates, huku Arsenal wakiishia kumaliza kwenye nafasi ya nne na kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya ambako wataanzia kwenye hatua ya mtoano, walimaliza mbele ya Tottenham.

Van Persie alishinda taji lake la kwanza la Ligi akiwa na miaka 29, hii ni baada ya miaka karibu 10 ndani ya Ligi Kuu England. Siku ambayo timu hiyo ilikuwa ikipitisha ubingwa kwenye mitaa ya Jiji la Manchester, hakuna ubishi kuwa Mholanzi huyo alikuwa hajutii maamuzi yake ya kung’ang’ania kuondoka Arsenal.
Lakini miezi au miaka kadhaa anaweza kubadilika kwa kile anachokifikiria kuhusu uamuzi wake wa kuondoka Emirates.

Arsenal imekuwa ikibanwa na mkataba wa ufadhili wa Uwanja wa Emirates na Wenger (kwa hiyari yake) amekuwa akibana matumizi ya klabu hiyo kila dirisha la usajili linapofunguliwa. Lakini hali sasa hivi inabadilika.
Arsenal wanahusishwa na usajili wa mastaa kama Gonzalo Higuain kutoka Real Madrid, Marouane Fellaini kutoka Everton na hata staa mwenzake Van Persie pale Old Trafford, Wayne Rooney. Kumekuwa na mabadiliko kwenye suala la matumizi na rasilimali, bata zote sasa hivi ziko Arsenal na kama angebaki kwa msimu mmoja zaidi angeshiriki kwenye kula bata pande za Emirates.

Huku Old Trafford alipo sasa hivi timu iko kwenye kipindi cha mpito, kipindi cha kusahau utawala wa Ferguson na kuingia kwenye zama za utawala wa David Moyes.
Kuna uwezekano mkubwa sasa kwa kiwango cha Manchester City kupanda chini ya kocha mpya Manuel Pellegrini, ambaye tayari ametumia kiasi cha pauni milioni 45 kwa kuwaleta Etihad, Fernandinho na Jesus Navas halafu bado wanaweza kununua zaidi kwa sababu dirisha la usajili bado sana kufungwa.

Jose Mourinho amerudi kuiongoza Chelsea, ni wazi kuwa atatoa upinzani mkali kwa Man United msimu ujao. Yote kwa yote uwezekano wa Man United kutetea ubingwa wao ni mdogo zaidi msimu ujao. Kumekuwa na mabadiliko makubwa sana, siyo Old Trafford tu, bali kwenye timu zote zilizomaliza ‘top 4’ msimu uliopita.

Arsene Wenger, mlezi wa Van Persie bado yuko Arsenal amechukua cheo cha kocha aliyedumu kwa muda mrefu zaidi na timu kwa sasa, baada ya Fergie kuondoka. Arsenal wanafedha ya kutumia na wanatarajiwa kutoa upinzani wa kweli kwenye ubingwa msimu ujao.

Tukiwa wa kweli katika ishu hii, ni ngumu kuamini iwapo Van Persie kuna siku atajutia kuondoka Arsenal, watu wanaamini kuwa aliondoka kwa sababu alikuwa akiamini alikuwa ameshapata kila alichotaka akiwa The Gunners na alikuwa akitafuta kubadilisha mazingira. Mwenyewe alisema aliondoka Emirates kwa sababu alikuwa akitaka mataji na amepata moja tayari.

Hata hivyo, ni ngumu kuamini kama amepata kile alichokitaka kutoka kwa Ferguson pale Old Trafford, watu wanahofu huenda akawa anajuta kwa sababu Van Persie hakupata muda wa kutosha wa kujifunza kutoka kwa kocha huyo aliyeachana na soka.

Kama mataji yakiendelea kutua Old Trafford chini ya David Moyes hatojutia uamuzi wake, lakini iwapo Chelsea, Man City na hata Arsenal wakifanikiwa kuitoa Man United kwenye ufalme wa England, RVP anaweza kujikuta anajuta kutokana na kushindwa kupata mataji mengi zaidi kama alivyotarajia wakati akitua Man United.

RVP anaweza kujiona kama mtu aliyepishana na gari la mshahara, kwa kuja Man United kipindi ambacho Ferguson anakaribia kustaafu na Arsenal wanaachana na ubahili, huku kukiwa na kila dalili za mafanikio kuhamia Emirates.


No comments:

Post a Comment