Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

BOBAN: "KASEJA AKIJA COASTAL UNION NAONDOKA"


BAADA ya Juma Kaseja kutemwa katika usajili wa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa klabu hiyo, Zakaria Hanspope, ameanika sababu za kushindwa kumwongeza mkataba mpya, huku kiungo mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo aliyetua Coastal Union, Haruna Moshi ‘Boban’ akisema hayupo tayari kucheza naye kikosi kimoja.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Hanspope alisema Kaseja alikuwa akiwapiga chenga walipomhitaji kufanya naye mazungumzo baada ya mkataba wake kufikia ukingoni.

Hanspope alisema walimwita ili kufikia mustakabali wake wa kuendelea kuichezea timu hiyo, lakini hakuwa tayari na baadaye waliamua kuachana naye, wakiamini amepata timu nyingine.
Hanspope alisema Mei mwaka huu, walimwita kwa ajili ya mazungumzo lakini hakuitika wito huo, kwa madai alikuwa katika majukumu ya timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, na ilikuwa inakabiliwa na mechi mbili za kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia.

Taifa Stars ilikuwa na mechi ngumu dhidi ya Morocco, ambapo ilifungwa mabao 2-1, katika mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye Uwanja wa Stade de Grand mjini Marrakech na baadaye ilizamishwa na Ivory Coast mabao 4-2, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kaseja ambaye mkataba wake ulimalizika rasmi jana, baada ya kuichezea timu hiyo tangu mwaka 2002 akitokea Moro United, mara ya mwisho kukutana na mwenyekiti wa usajili wa klabu hiyo, ilikuwa wakati Stars ikijiandaa kucheza na Morocco.

 “Nilimwambia Kaseja sisi bado tuna nia ya kuendelea na wewe msimamo wako ni upi? Alinijibu hawezi kusema lolote kwa kuwa alikuwa katika majukumu ya timu ya taifa, akimaliza atanijibu,” alisema Hanspope.

Alisema aliendelea kuwa na msimamo wake usioeleweka baada ya kumaliza majukumu ya kuitumikia timu ya taifa, ikiwa ni zaidi ya wiki mbili, hakuwahi kukaa katika meza moja ya mazungumzo na uongozi wa klabu hiyo licha ya kumtaka kufanya hivyo.

Hanspope alisema waliamini kwamba, amemaliza mkataba wake na wanamwita hataki labda alikuwa na mipango yake mingine na waliamua kumwacha ili aendelee na utaratibu wake.
Hata hivyo, alisema uwezo wa Kaseja umeshuka mno tofauti na ilivyokuwa katika miaka ya nyuma, hali inayompa wakati mgumu kwa mashabiki wa timu hiyo.

 Msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara, mashabiki walitaka kumpiga baada ya kufungwa na Mtibwa Sugar mabao 2-0, katika mchezo wa kwanza, uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Wakati huo huo, Kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ aliyesajiliwa na Coastal Union katika majira haya ya joto kwa mkataba wa msimu mmoja, ameeleza kuwa hataki kumwona Kaseja akijiunga na timu hiyo.

Habari zilizopatikana jana kutoka kwa marafiki wake wa karibu LENZI YA MICHEZO kuzinasa, zilidai kwamba Boban amechukizwa na mambo aliyofanyiwa na Kaseja wakati akiwa nahodha wa Simba wa muda mrefu na ameweka wazi kuwa endapo atajiunga na Coastal, yeye ataacha kuichezea miamba hiyo ya Tanga.

Boban ni miongoni mwa wachezaji wa Simba waliotemwa na klabu hiyo, wengine wakiwa ni Felix Sunzu na Amir Maftah, baada ya mikataba yao kumalizika huku Juma Nyosso, Abdallah Juma na Paul Ngalema wakishindwa kuomba kuvunja mikataba yao miamba hiyo ya Msimbazi.


No comments:

Post a Comment