Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 30, 2013

NIZAR KHALFAN NA OSCAR JOSHUA WAJITIA KITANZI

Nizar Khalfan (kulia)

KIUNGO wa Yanga, Nizar Khalfan na beki wa timu hiyo, Oscar Joshua wameendelea kuula baada ya kuongezwa mikataba mipya kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku Shadrack Nsajigwa akitemwa kwenye kikosi hicho.

Msimu uliopita Nsajigwa aliongezwa mkataba wa mwaka mmoja, baada ya kuichezea timu hiyo kwa muda mrefu akitokea Moro United, hata hivyo, LENZI YA MICHEZO ina taarifa kwamba anatarajiwa kupewa jukumu la kuwa kocha msaidizi wa timu hiyo.

Nsajigwa wiki iliyopita alimaliza kozi ya ngazi ya pili ya ukocha iliyoandaliwa na Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), itakayomwezesha kukaa kwenye benchi la ufundi la timu hiyo katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.

 Habari zilizopatikana Dar es Salaam kutoka ndani ya Kamati ya Usajili iliyochini ya Mwenyekiti wake, Abdallah Bin Kleb, zilieleza Joshua na Nizar wameongezewa mkataba kwa kuwa bado wana mchango mkubwa katika kikosi cha timu hiyo.

Chanzo hicho kilieleza kwamba, wachezaji hao wameongezewa mkataba kutokana na mapendekezo ya Kocha Mkuu wa timu hiyo, Ernie Brandts, aliyeiwezesha Yanga kuchukua ubingwa msimu uliopita.

 “Wachezaji hao mikataba yao ilikuwa imemalizika, tumeamua kuwaongezea ili waweze kuisaidia timu yetu katika msimu ujao wa ligi kuu na Ligi ya Mabingwa mwakani,” kilieleza chanzo chetu.
Kilieleza kwamba baadhi ya wachezaji akiwemo Stephano Mwasyika, Godfrey Taita, Said Mohamed, hawajaongezewa kutokana na mikataba yao imemalizika huku wakionekana si msaada tena kwa timu.

Wakati huo huo, Brandts anatarajia kutua nchini leo  akitokea kwao Uholanzi alikokuwa kwenye mapumziko, baada ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ambao ni mabingwa wa ligi hiyo, wanatarajia kuanza mazoezi kesho kujiandaa na msimu ujao.


No comments:

Post a Comment