Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, June 2, 2013

ABAJALO YAFUNGISHWA VIRAGO NA KARIAKOO YA LINDI LEO, ILULU

TIMU ya Abajalo ya Dar es Salaam leo imetolewa kwenye mashindano ya bingwa wa mikoa baada ya kufungwa bao 1-0 na Kariakoo Lindi.

Mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani ulichezwa kwenye Uwanja wa Ilulu mjini Lindi, na wenyeji kufanikiwa kutumia Uwanja wao vema na kufanikiwa kusonga hatua ya tatu.

Akizungumza kwa njia ya simu toka Lindi, Mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa Lindi (LIREFA), Francis Ndulane alisema kuwa bao hilo lilifungwa na mshambuliaji Salum Abilah kipindi cha kwanza baada ya kuwazidi mbio mabeki wa Abajalo.

“Mchezo umemalizika na Kariakoo Lindi wamefanikiwa kusonga mbele baada ya kuifunga Abajalo bao 1-0 lililofungwa na Salum Abilah kwa shuti kali lililomshinda golikipa wa Abajalo baada ya kuwazidi mbio mabeki”, alisema Ndulane.

Kariakoo inayofundishwa na Nyamwase Rashid kwenye mchezo wa ugenini Dar es Salaam walilazisha sare ya mabao 2-2 kwani walitoka nyuma wakiwa wamefungwa mabao 2-0 na kufanikiwa kusawazisha zote na kuahamsha matumaini ya kusonga mbele.


Abajalo inakuwa timu ya pili toka Dar es Salaam kuaga mashindano haya baada ya Friends Rangers kutolewa kwenye hatua ya kwanza.

No comments:

Post a Comment