Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, May 3, 2013

RUAHA, CDTI, MKWAWA NA TUMAINI UNIVERSITIES KUONYESHANA KAZI KWENYE POOLTABLE T


Mashindano ya mchezo wa pool table kwa vyuo vikuu yataanza kutimua vumbi kesho mjini Iringa na yatafanyika kwenye Ukumbi wa Twisters Club.

Jumla ya Vyuo vikuu vinne vilivyopo Iringa vitashiriki ambavyo ni Ruaha, CDTI, Mkwawa na Tumaini na vimeshakabidhiwa vifaa vya mashindano.

Akizungumza na LENZI YA MICHEZO kwa njia ya Simu toka Iringa, Mwenyekiti wa chama cha mchezo wa Pool mkoa wa Iringa (IRPA), Salim Kisaku amesema kuwa mashindano hayo yatakayoshirikisha vyuo vikuu vinne ambavyo ni Ruaha, CDTI, Mkwawa na Tumaini.

“Mashindano ya pool yataanza kesho na vyuo vikuu vya Ruaha, CDTI, Mkwawa na Tumaini ndio vitakavyoshiriki na vimeshachukuwa vifaa vya mashindano ambavyo ni pool table, na vifaa vyake vyote na fulana na kofia ambazo watavaa washiriki”, alisema Kisaku

Pia amesema chuo kitakachobeba ubingwa wa mkoa huo ndicho kitakacho shiriki katika fainali za taifa za mashindano hayo zitakazofanyika Juni mosi, mwaka huu jijini Dar es salaam.

Bingwa wa mashindano hayo kwa upande wa timu katika ngazi ya mkoa atajinyakulia fedha taslim Sh.500,000, mshindi wa pili Sh.300,000, mshindi wa tatu Sh.200,000 na mshindi wa nne Sh.100,000.
Kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume) bingwa atazawadiwa Sh.150,000 na mshindi wa pili Sh.100,000 wakati kwa upande wa wanawake bingwa atapewa Sh.100,000 na mshindi wa pili Sh.50,000.

No comments:

Post a Comment