Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, November 12, 2012

ZAHA KUZIBA PENGO LA ROONEY ENGLAND




WINGA wa Crystal Palace mwenye thamani ya pauni milioni 20, Wilfried Zaha (20) amejumuishwa kwenye kikosi cha England, kitakacho cheza pambano la kirafiki dhidi ya Sweden, Jumatano hii.
Wayne Rooney, Theo Walcott, Jonjo Shelvey, Kyle Walker, Aaron Lennon, Jermain Defoe na Alex Oxlade-Chamberlain watakosa mechi hiyo itakayochezwa Stockholm, Sweden kutokana na majeruhi.


Kutokana na kukosekana kwa wachezaji hao, Roy Hodgson ameamua kumuita kinda huyo mzaliwa wa Ivory Coast kuziba baadhi ya nafasi zilizoachwa na mastaa hao.
Zaha amekuwa akitajwa kama mmoja wa wachezaji wenye vipaji vikubwa sana anayeibukia kwenye soka la England na amekuwa akihusishwa kujiunga na klabu kadhaa kubwa za ligi kuu huku Arsenal wakionekana kuongoza mbio za kumsajili.

No comments:

Post a Comment