Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, November 12, 2012

MANATSA NDIE BINGWA WA MICHUANI YA JOHNNIE WALKER WAITARA 2012

Mshindi wa jumla wa mashindano ya kombe la Johnnie Walker Waitara 2012 Sudson Manatsa akinyanyua juu vikombe vyake viwili alivyoshinda wakati wa Mashindano hayo yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gofu Lugalo jijini Dar es Salaam. Mashindano hayo yalidhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti kupitia kinywaji chake kikali cha Johnnie Walker

Mgeni rasmi wa Mashindano ya Johnnie Walker Waitara Trophy,  Mlezi wa Gofu nchini Kenya na Mkurugenzi wa ICEA LION, Dunkan Nderitu Ndengwa kutoka nchini Kenya  akimkabidhi zawadi Mshindi wa jumla wa mashindano ya  kombe la Johnnie Walker Waitara 2012 Sudson Manatsa. Kampuni ya Bia ya Serengeti ilidhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Johnnie Walker.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Stephen Gannon  akimkabidhi zawadi Mshindi wa pili wa  daraja A, Aidan Nziku  kikombe na zawadi nyingine baada ya kuibuka mshindi wa kundi hilo katika mashindano ya kuwania kombe la Johnnie Walker Waitara 2012. Kampuni ya Bia ya Serengeti ilidhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Johnnie Walker.

No comments:

Post a Comment