Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 29, 2012

SIMBA IPO KAMILI

KIKOSI CHA SIMBA
Mshambuliaji wa SIMBA Christopher Edward


TIMU ya Simba leo majira ya saa 11 jioni itacheza na Prison ya Mbeya uwanja wa Taifa bila mshambuliaji wao wa kimataifa toka Uganda Emanuel Okwi ambaye anatumikia adhabu yake ya kadi nyekundu aliyoonyeshwa kwenye mchezo dhidi ya JKT Ruvu.

Okwi alimpiga kiwiko Kessy Mapande wa JKT Ruvu wakati mpira ukiwa haupo mchezo hivyo. Kufuatana na sheria za soka, sheria namba 12 ambayo inasema tabia mbaya mchezoni kwenye makosa makubwa saba ambayo mchezaji anaonyeshwa kadi nyekundu  Okwi alifanya kosa ambalo lipo kwenye violet conduct na kufuatana na sheria  alipashwa kukosa mechi mbili tu lakini kanuni zinazoendesha ligi ya Tanzania zimeongeza adhabu kuwa mechi tatu na faini

Pia mshambuliaji huyo atakosa mchezo wa Simba na Yanga utakaochezwa Octoba 3 mwaka huu uwanja wa Taifa.

Washambuliaji chipukizi wa Simba Shomari Kapombe na Christopher Edward wamewatoa wasiwasi mashabiki kwa kusema wao wakae mkao wa kukesha siku hiyo maana wataleta furaha Msimbazi kwa kuhakikisha wanatoka na pointi 3.

Washambuliaji hawa wamekuwa ndio habari ya mjini kwa sasa kutokana na kandanda wanalosakata kuwa lakiustadi zaidi

No comments:

Post a Comment