SERIKALI YAJIVUNIA UIMARA WA UCHUMI



Serikali imepata mafanikio makubwa katika kusimamia uchumi wa nchi ambapo Pato la Taifa limeendelea kukua kwa kasi ya asilimia 5.1 mwaka 2024, huku mfumuko wa bei ukidhibitiwa kubaki ndani ya lengo la asilimia 3.0 hadi 5.0, hali inayotoa ahueni kwa maisha ya Watanzania.

Mafanikio haya yameenda sanjari na hatua ya kihistoria ya kuzindua mchakato wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ambayo sasa inatoa mwelekeo mpya wa nchi kuelekea uchumi wa kipato cha juu ifikapo nusu ya karne. OUA YA BAJETI YA OFI YA

Hayo yamesemwa na  Profesa Kitila Mkumbo wakati akisoma Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Bungeni leo.

Prof Kitila pia alisema kwamba Serikali katika kuimarisha uwekezaji, imefanikiwa kusajili miradi ya uwekezaji yenye thamani ya dola za Marekani bilioni 5.48 kupitia Kituo cha Uwekezaji (TIC), hatua iliyochochewa na maboresho ya sera na sheria yaliyofanywa kwa makusudi ili kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha biashara na uzalishaji katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

Sambamba na mafanikio hayo, usimamizi wa Mashirika ya Umma umeshuhudia mageuzi makubwa ambapo Ofisi ya Msajili wa Hazina imefanikiwa kukusanya mapato yasiyo ya kodi ya kiasi cha shilingi bilioni 773.37 hadi kufikia Machi 2026, ikiwa ni ongezeko la asilimia 16 ndani ya mwaka mmoja.

Aidha Serikali imefanikiwa pia kukamilisha mapitio ya mfumo wa kisheria wa uwekezaji wa umma na kuunganisha baadhi ya taasisi ili kuongeza tija na kupunguza mzigo wa gharama za uendeshaji kwa mlipa kodi.

Aidha, kuanzishwa kwa Maeneo Maalum ya Kiuchumi (SEZ) kumeleta matokeo chanya kwa kusajili miradi inayotoa ajira kwa vijana na kukuza mauzo ya bidhaa nje ya nchi, jambo ambalo limeimarisha akiba ya fedha za kigeni na kuifanya nchi kuwa na ustahimilivu wa kiuchumi licha ya changamoto za kijiopolitika duniani.

Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji imeliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi bilioni 174.59 kwa ajili ya mwaka wa fedha 2026/27. Kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 94.67 zimepangiwa matumizi ya kawaida yakijumuisha mishahara na uendeshaji wa ofisi, huku shilingi bilioni 79.91 zikielekezwa moja kwa moja kwenye miradi ya maendeleo

No comments