AFCON 2025 YAJA,AFRIKA MASHARIKI WATAKIWA KUITHAMINI
Kuelekea kuanza kwa Fainali za
Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2025) nchini Morocco, viongozi wa masoko ya
burudani wamehimiza nchi za Afrika Mashariki (E.A) kuacha kusherehekea ligi za
mataifa mengine na kuelekeza nguvu zao katika kuthamini na kuwekeza katika
mashindano haya makubwa ya soka barani Afrika.
Mashindano ya
AFCON 2025 yanatarajiwa kuanza Januari 21 na kumalizika Februari 18 nchini
Morocco, ambapo mechi zote 52 zitaoneshwa mubashara kupitia SuperSport.
Akizungumza
Dar es Salaam, Meneja wa Masoko wa Kampuni ya Multchoice Tanzania, Baraka
Shelukindo, alisisitiza umuhimu wa kukuza utambulisho wa Kiafrika kupitia
soka.
"Haya
ni mashindano ya Afrika, tusherehekee Uafrika wetu," amesema
Shelukindo.
AFCON:
Zaidi ya Soka, Ni Utamaduni
Shelukindo alieleza
kuwa Multchoice imeonesha dhamira ya dhati kwa kurusha mechi zote, akibainisha
kuwa AFCON sio tu mashindano ya soka bali ni tukio linalobeba utamaduni,
historia, na umoja wa Waafrika.
Kwa kutambua
hilo, matangazo ya mashindano hayo yataenda kwa lugha mbalimbali, ikiwemo Kiswahili,
Kiingereza, Kifaransa, na Kireno, ili kuwafikia kila shabiki barani.
Kwa Tanzania,
ambayo ipo Kundi C, mechi zake zitapatikana kupitia kifurushi cha Bomba,
ikiwa ni mkakati wa kuwafikia mashabiki wengi zaidi na kuwawezesha kuungana na Taifa
Stars yao.
Daraja
la Kibiashara na Maskauti wa Ulaya
Mbali na
burudani na umoja, Shelukindo alisisitiza jinsi AFCON inavyotumika kama daraja
muhimu la kiuchumi na kimasoko kwa wachezaji wa Afrika.
"AFCON
inatumika kama jukwaa kwa wachezaji chipukizi na wale wanaong’ara barani
kuonesha vipaji vyao kwa maskauti wa Ulaya wanaofuatilia kwa karibu michuano
hii," alisema.
Alisisitiza
kuwa kwa Tanzania, huu ni wakati wa kipekee kwa wachezaji wa Taifa Stars kujitangaza
na kufungua milango ya kucheza Ligi kubwa Ulaya.
Hoja
ya Kuthamini Mashindano Yetu
Hoja ya
msingi iliyotolewa na Shelukindo inatutaka tuwekeze hisia na rasilimali zetu
katika AFCON badala ya ligi za nje. Hii ndio sababu ya kimsingi ya kuthamini
AFCON:
1. Kukuza Utambulisho: Kusherehekea AFCON ni kusherehekea
utambulisho wa Kiafrika na kujitambulisha kama taifa moja kupitia soka,
kuachana na tabia ya kuiga kwingine.
2. Fursa za Kiuchumi za Ndani: Kuthamini AFCON kunahamasisha matumizi
ya ndani (kulipia vifurushi vya ndani, kutazama kwa pamoja), tofauti na
ligi za nje ambazo faida zake huishia Ulaya.
3. Kuongeza Thamani ya Wachezaji: Mashindano haya ndio njia pekee wachezaji
wa Tanzania na Afrika kupandisha thamani yao na kupata mikataba mikubwa nje ya
nchi.
4. Ujenzi wa Umoja wa Familia: "Msimu wa AFCON ni wakati wa familia
nzima kukutana, kuungana na kusherehekea utambulisho wa Kiafrika kupitia soka.
Ndio maana tumesema, wanafamilia tuna kikao chimbo – ni DStv,"
alihitimisha Shelukindo, akihimiza matumizi ya vifurushi vya ndani.
Post a Comment