FUTSAL: Timu ya Wanawake Yafunga Kambi Indonesia, Yajiandaa Kuweka Historia Kombe la Dunia Ufilipino
Timu ya taifa ya mchezo wa Futsal ya Wanawake imekamilisha kambi yake ya
maandalizi ya wiki moja mjini Jakarta, Indonesia, na leo inatarajiwa kuelekea
Manila, Ufilipino, kwa ajili ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia la Futsal.
Tanzania
inashiriki michuano hiyo mikubwa kwa mara ya kwanza kabisa baada ya kunyakua
nafasi ya pili kwenye michuano ya Afrika iliyofanyika Morocco Mei, mwaka huu.
Timu Imeimarika
Siku Hadi Siku
Kocha Mkuu wa
timu hiyo, Curtis Reid, alisema kambi hiyo ilikuwa na manufaa makubwa,
akitoa shukrani kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kufanikisha
maandalizi hayo. Katika kambi hiyo iliyoanza Alhamisi iliyopita, timu ilicheza
mechi nne za kirafiki.
"Nimefurahi
kupata kambi ya Indonesia, imenisaidia sana kuimarisha wachezaji wangu,
naishukuru TFF kwa kutekeleza hili," alisema Kocha Reid.
Aliongeza kuwa
ameridhishwa na mwitikio wa wachezaji wake katika mazoezi na mechi za kirafiki.
"Umeona
timu ilivyocheza mechi ya kwanza ilikuwa tofauti kwenye mechi ya pili, na ya
tatu na hata hii ya nne. Naweza kusema timu imeimarika na ninaamini tutakuwa na
michuano mizuri Manila,"
alisema kwa uhakika.
Lengo ni
Kujifunza na Kupata Uzoefu
Kocha Reid
alifafanua kuwa kikosi kinachoshiriki Kombe la Dunia kina sura nyingi mpya.
Wachezaji wengi wanaounda kikosi hicho si wale walioshiriki michuano ya Afrika
Morocco. Hii inatokana na wachezaji wengi wa awali kuwa kwenye klabu yao ya JKT
ambayo ilishiriki michuano ya klabu bingwa Afrika.
"Hawa
wachezaji wengi ni wapya si wale waliokuwa na timu kwenye michuano ya Afrika
Morocco. Mechi hizi za kirafiki ndio mechi zao za kwanza kucheza. Tukienda
kwenye Kombe la Dunia naamini watazidi kujifunza na kupata uzoefu zaidi," alisisitiza Reid, akifafanua kuwa lengo
kuu ni kuendelea kuwajengea uwezo wachezaji hao.
📅 Ratiba Ngumu Kundi C
Tanzania
imepangwa Kundi C katika michuano hiyo inayoshirikisha timu 16. Imepangwa
pamoja na timu zenye nguvu za Ureno, Japan, na New Zealand.
Ratiba ya
Tanzania katika hatua ya makundi ni kama ifuatavyo:
·
Novemba
23: Tanzania vs. Ureno
·
Novemba
26: Tanzania vs. New
Zealand
·
Novemba
29: Tanzania vs. Japan
Timu
inatarajia kuweka historia na kupata uzoefu wa thamani itakapokuwa inaanza
kurusha kete yake ya kwanza dhidi ya Ureno.
Post a Comment