CRISTIANO RONALDO AWEKA REKODI YA KUWA BILIONEA WA KWANZA KISOKA DUNIANI!
Hadithi ya soka
imeandikwa upya! Cristiano Ronaldo, gwiji wa Ureno na mshambuliaji wa
klabu ya Al-Nassr ya Saudi Pro League, sasa amekuwa mwanasoka wa kwanza kabisa
katika historia kufikia hadhi ya bilionea duniani, kwa mujibu wa kampuni
ya habari na kifedha ya Bloomberg.
Faharasa ya
Mabilionea ya Bloomberg, ambayo hufuatilia utajiri wa watu matajiri zaidi
duniani kulingana na mali zao halisi, imepima utajiri wa mchezaji huyo mwenye
umri wa miaka 40 kwa mara ya kwanza na kuthibitisha kwamba sasa ana utajiri
halisi wa Dola bilioni 1.4 (takriban Shilingi trilioni 3.5 za Tanzania).
Hesabu hii
inazingatia mapato yake yote ya kazi, uwekezaji, na mikataba ya matangazo.
Taarifa hiyo
inaonesha kuwa Ronaldo alijikusanyia zaidi ya Dola milioni 550 (takriban
Shilingi bilioni 1.37) kupitia mshahara pekee kati ya mwaka 2002 na 2023. Zaidi
ya hayo, inabainisha mikataba yake mikubwa ya udhamini, ikiwemo mkataba wa
miaka kumi na kampuni ya Nike wenye thamani ya takriban Dola Milioni 18
(Shilingi Bilioni 45) kwa mwaka.
Mambo yalimwendea
vyema zaidi Ronaldo alipojiunga na Al-Nassr mwaka 2022, ambapo inaripotiwa kuwa
alipata mshahara mkubwa zaidi katika historia ya soka duniani, ukiwa na thamani
ya takriban Pauni milioni 177 kwa mwaka.
Hivi karibuni, alitia
saini mkataba mpya wa miaka miwili wenye thamani ya zaidi ya Dola milioni
400 (takriban Shilingi trilioni 1), ambao unamfanya abaki klabuni hapo hata
baada ya kutimiza umri wa miaka 42.
Messi
Naye Yuko Karibu
Licha ya Ronaldo
kupiga hatua hii kubwa, mpinzani wake wa jadi, Lionel Messi,
mshambuliaji wa Argentina na Inter Miami, naye yuko kwenye ramani ya matajiri.
Bloomberg inasema
Messi, mwenye umri wa miaka 38, amepata zaidi ya Dola milioni 600 (takriban
Shilingi bilioni 1.5) katika mshahara kabla ya kodi katika kipindi chote
cha maisha yake ya soka.
Hata hivyo, mapato
yake ya sasa ya Inter Miami, ambapo anapata takriban Dola milioni 20 kwa mwaka,
ni asilimia 10 tu ya kile ambacho Ronaldo anakipata Al-Nassr katika
kipindi hicho hicho.
Ikumbukwe kwamba
Messi, atakapostaafu, anatarajiwa kupata hisa katika klabu yake ya Inter
Miami, hatua itakayomweka kwenye orodha ya matajiri wakubwa wa michezo kwa
miaka mingi ijayo.

Post a Comment