Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, October 6, 2017

TAIFA STARS TAYARI KUIKABILI MALAWI KESHO

Kocha wa timu ya Taifa ya Soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Mayanga (katikati) akizungumza na wandishi wa habari jana kuhusu mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Malawi unaotarajiwa kuchezwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Kulia ni nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta na kocha wa Malawi Ronny Van Geneugden. 

Kocha wa timu ya Taifa ya Soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Mayanga (wa pili kulia) akizungumza na wandishi wa habari jana kuhusu mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Malawi unaotarajiwa kuchezwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Kulia ni nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta, kocha wa Malawi Ronny Van Geneugden (wa pili kushoto) na nahodha wa Malawi Robert Ng’ambi.
TIMU ya taifa ya soka ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kesho inatarajia kushuka katika dimba la Uhuru, Dar es Salaam kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga alisema wamejiandaa vema kwani anaamini mchezo utakuwa na ushindani kwa sababu Malawi wamewaita nyota wake wanaocheza soka nje ya nchi yao.
“Tunataka ushindi ili tuzidi kupanda katika viwango vya FIFA hadi tufike kwenye tarakimu mbili, najua mchezo utakuwa na ushindani lakini tumejiandaa kushinda,” alisema Mayanga.
“Wamebadilisha kikosi kwa kiasi kikubwa, kwa maana hiyo hatupaswi kuwadharau licha ya matokeo mazuri tuliyopata dhidi yao kwenye mechi za COSAFA,” alisema Mayanga ambapo Taifa Stars iliifunga mabao 2-0 katika mchezo huo
Naye nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ameonyesha kujiamini na kuwataka Watanzania kwenda uwanjani wakiwa na uhakika wa kufurahi.
 “Watanzania waje uwanjani, wengine watutazame kwenye televisheni wakiwa na uhakika timu yao itapata ushindi kesho (leo),”.
“Wachezaji wote wana morali na viwango vyao mazoezi ni vikubwa, na cha zaidi nawahakikishia mimi binafsi nipo kwenye kiwango bora kabisa,” alisema Samatta.
Naye kocha wa Malawi, Ronny Van Geneugden alisema anaifahamu Taifa Stars kwasababu walicheza nayo kwenye mashindano ya COSAFA hivyo wamejiandaa kurudisha kipigo walichopata Afrika Kusini.
“Nimeshaifahamu Tanzania na namna timu za Afrika zinavyocheza hivyo safari hii tutalipiza kisasi baada ya kutufunga katika mashindano ya COSAFA,” alisema Van Geneugden Mbeligiji huyo ambaye alianza kuifundisha Malawi Aprili mwaka huu.

Katika viwango vya Fifa vilivyotoka mwezi uliopita Malawi inashika nafasi ya 116 na Tanzania inashika nafasi ya 125.

No comments:

Post a Comment