WAKALI wa kusakata
kambumbu waliowahi kuchezea timu ya Bandari ‘Bandari Veterani’ wanatarajiwa
kushuka dimbani kucheza na timu ya Bandari kesho kwenye uwanja wa Bandari
Kurasini, Dar es Salaam.
Akizungumza na gazeti hili jana, mratibu wa
mechi hiyo Kenedy Mwaisabula maarufu kama ‘Mzazi’ alisema mchezo huo wa
kufungua mwaka 2017 utaanza saa mbili asubuhi na kuwaalika wapenzi wa soka
kujionea vipaji.
“Mchezo utakuwa wa kuvutia kwani wakongwe
watakuwa na kazi ya kuwafundisha vijana namna ya kucheza soka bila kukimbizana
kwani watakuwa wanapipiga pasi moja na kuachia hivyo nawaalika wote kwani
hakuna kiingilio,” alisema Mwaisabula.
Kikosi cha Bandari cha zamani kitaundwa na
wachezaji Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Salvatory Edward, Salum Sued ‘Kusi’,
Waziri Mahadhi ‘Mandieta’, Semmy Kessy, David Beatus, Mudy Pwani, Zuberi
Katwila, Gwakisa Mwandambo.
Wengine ni Simon Butte,Juma Dallo, Jemedari Said, Husein Mataka,
Mick Zongela, Peter Nkwera, Ismail Issa, Rajab Kablao na Abdallah Rajab.
Pia
Mwaisabula alisema mchezo huo utakuwa sehemu ya kuwakutanisha wakongwe hao na
kubadilishana mawazo, kwani wengi wao inakuwa nadra kuonana baada ya kuachana
kwenye soka la ushindani na baadae watashiriki kwenye sherehe ya kukaribisha
mwaka itakayofanyika Bandari.
Samia aweka shada kaburi la askari asiyefahamika
-
Na Beda Msimbe, TBN,Moscow
KENGELE kubwa iliyogongwa mara tisa, bendi ya jeshi ikiongoza nyimbo za
maombolezo Rais Samia Suluhu Hasan majira ya saa ta...
CCM kuna Yuda au ni homa ya urais 2030?
-
Mitandao ya kijamii nchini Tanzania imelipuka kwa mjadala kuhusu jina moja
tu - "Yuda". Limeibuliwa na mwanasiasa Simai Mohammed Said. Yuda ni nani?
Kwanin...
Welcome to the Jungle: Arusha’s Wildest Afternoon
-
Most safari guides tell you to head straight to the Serengeti. But if you
want a wild, unfiltered, face-to-face encounter with Africa’s finest in
jus...
NI SIMBA QUEENS MABINGWA LIGI YA WANAWAKE TZ BARA
-
TIMU ya Simba Queens imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Soka ya
Wanawake Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Mashujaa
Queens jion...
WASIRA AWATOLEA UVIVU WALIOANZA MBIO ZA URAIS
-
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Stephen
Wasira, Leo Machi 27, 2026, Mjini Bunda Mkoa wa Mara alipokuwa akiweka
jiwe la ms...
Post a Comment