Adhabu hiyo imetokea kufuatia yaliyojiri wakati wa ushindi wa West Ham wa 2-1 dhidi ya Chelsea uwanjani Upton Park Oktoba 24.
Wachezaji watano wa Chelsea walilishwa kadi za manjano na na kiungo wa kati Nemanja Matic na meneja Jose Mourinho walifukuzwa uwanjani.
Wachezaji wa West Ham walimzingira refa Jonathan Moss baada ya Matic kumkaba Diafra Sakho dakika ya 44.
“Shtaka lilihusu kukosa kuhakikisha wachezaji wanadumisha nidhamu uwanjani,” FA imesema kupitia taarifa.
Wachezaji wa Chelsea pia walimzingira refa baada ya Matic, aliyeonyeshwa kadi ya njano awali, kupewa kadi nyingine ya njano na Moss na kufukuzwa uwanjani.
Alipigwa marufuku uwanjani mechi moja na kupigwa faini ya £40,000.
No comments:
Post a Comment