Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, April 11, 2015

MKWASA AJIGAMBA KUIFUNGA MBEYA CITY MABAO 12





“SIKU hizi sisi tunakwenda na idadi ya siku tu hivyo kesho tunatarajia mabao 12” Hayo ni maneno ya Kocha msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa aliyokuwa akimwambia Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka Nchini (TFF) Salum  Madadi alipokuja kumsalimia wakati wa mazoezi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume zilipo ofisi za TFF.

Kauli hiyo ilikuja baada ya Madadi kumtania Mkwasa akimwambia juzi tarehe 8 mlishinda mabao maneno dhidi ya Coastal Union na kesho tarehe 12 tutarajie nini? Ndipo Mkwasa alipomjibu siku hizi sisi tunakufunga kwa idadi ya tarehe ya siku husika hivyo kesho (leo) tunafunga mabao 12 na kuachia kicheko kilichofuatiwa na kugongeana mikono.

Yanga imegeuka gumzo baada ya kuifunga Coastal Union ya Tanga mabao 8-0 kwenye mchezo uliopita ambao ulichezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kufanikiwa kuendelea kukaa kileleni ikiwa na pointi 43 baada ya kucheza mechi 19, pointi sita mbele ya mabingwa watetezi Azam FC wanaoshika nafasi ya pili.

Yanga leo asubuhi walifanya mazoezi mwisho kujiandaa na mchezo wao na Mbeya City kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam na kuvuta idadi kubwa ya watazamaji kama vile kuna mechi muda huu kwani walikuwa wakishangilia.

Wachezaji wa Yanga walionekana kuwa morali ipo juu na hakuna wanachohofia kwani kila mchezaji alionekena kufanya vizuri kwenye mazoezi hayo.

Wachezaji Juma Abdul na Dany Mrwanda walifanya mazoezi mepesi mepesi peke yao lakini Jerryson Tegete yeye hakufanya mazoezi kabisa kutokana na kuwa majeruhi muda mrefu.

No comments:

Post a Comment