Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, March 13, 2015

VIWANGO FIFA VYA UBORA DUNIANI: GERMANY NI NAMBA 1, ARGENTINA YA PILI, TANZANIA YAPANDA NAFASI 7 IPO YA 100.

MABINGWA wa Dunia, Germany, bado wapo Nambari Wani mbele ya Argentina na Colombia huku Tanzania ikipanda Nafasi 7 na kukamata Nafasi ya 100.
 Kwa Nchi za Afrika, Algeria ndio ipo juu ikiwa Nafasi ya 18 ikifuatiwa na Ivory Coast walio Nafasi ya 20.
 Italy wameingia 10 Bora kwa mara ya kwanza tangu Juni 2014 na kuwaporomosha Mabingwa wa Dunia wa zamani Spain ambao sasa wako Nafasi ya 11.
Listi nyingine ya Ubora Duniani itatolewa hapo Aprili 9.
KUMI BORA:
 1. Germany 
 2. Argentina 
 3. Colombia 
 4. Belgium  
 5. Netherlands 
 6. Brazil 
 7. Portugal  
 8. France  
 9. Uruguay  
10. Italy
 

Maeneo ya Tanzania:
 96 Oman 
 97 Iraq 
 98 Belarus 
 99 Saudi Arabia  
 100 Tanzania 
 101 Jordan 
 102 Antigua and Barbuda 
 102 Ethiopia  


Sare ya bao 1-1 iliyopata Tanzania dhidi ya Rwanda kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliochezwa jijini Mwanza imeisaidia kupanda kwa nafasi saba kwenye ubora wa viwango ambayo hutolewa na shirikisho la Soka Dunia (FIFA)

Kabla ya mchezo huo ambao ulikuwa ni kwa mujibu wa kalenda ya FIFA, Tanzania ilikuwa ikishika nafasi ya 107 lakini msimamo uliotolewa jana inashika nafasi ya 100.

Taarifa hiyo ambayo ipo kwenye wavuti ya FIFA inasema Nchi za Afrika ambazo zinashika nafasi za juu ni Algeria ambayo ni ya 18 ikifuatiwa na Ivory Coast ambayo ipo nafasi ya 20.

Nafasi ya kwanza imeemnelea kushikiliwa na Ujerumani, ambao ndio mabingwa wa dunia nafasi ya pili ikishikiliwa na Agentina huku nafasi ya tatu ikienda kwa Colombia
 Italy wameingia kwenye 10 ya dunia bora kwa mara ya kwanza tangu Juni 2014 na kuwaporomosha Hispania (Spain) ambao sasa wako nafasi ya 11.

Viwango vingine vya ubora vinatarajia kutolewa Aprili 9 mwaka huu

No comments:

Post a Comment