TIMU ya Polisi Morogoro imekatisha mkataba na kocha wake Mkuu,
Mohamed Adolph Rishaard kutokana na timu hiyo kucheza chini ya kiwango na kupoteza
michezo kwenye ligi Kuu..
Akizungumza kwa njia ya simu Mwenyekiti wa klabu ya Polisi Moro, Zuberi Chambera alisema kuwa kocha, Mohamed Adolph Richard amesitisha mkataba naye wa kuifundisha timu kutokana na kufanya vibaya na kusema maamuzi hayo yakifikiwa na kikao cha kamati ya utendaji ya timu.
Akizungumza kwa njia ya simu Mwenyekiti wa klabu ya Polisi Moro, Zuberi Chambera alisema kuwa kocha, Mohamed Adolph Richard amesitisha mkataba naye wa kuifundisha timu kutokana na kufanya vibaya na kusema maamuzi hayo yakifikiwa na kikao cha kamati ya utendaji ya timu.
“Ni kweli kocha wetu Mohamed Adolph Rishard amesimamishwa
kufundisha kutokana na sababu zilizotolewa na kupitishwa na kamati tendaji ni baada
ya kucheza chini ya kiwango tofauti na makubaliano yaliyofikiwa wakati wa mkataba
wetu”, alisema Chembera.
Polisi Moro imepoteza michezo minne, imetoka sare nane na kushinda michezo minne ya ligi kuu Tanzania bara na sasa timu ipo itanolewa na kocha msaidizi, John Tamba wakati wakisaka kocha mkuu mwenye sifa za kufundisha.
Naye Mohamed Rishard alisema kuwa kusitishiwa mkataba wake amelipokea kwa mikono miwili kutokana na timu kufanya vibaya kwani lilikuwepo moja ya kipengele kwenye mkataba kilitamka wazi endapo timu ingepoteza michezo mitatu kamati itamwita na kumhoji na wametekeleza kipengeleza
Polisi Moro imepoteza michezo minne, imetoka sare nane na kushinda michezo minne ya ligi kuu Tanzania bara na sasa timu ipo itanolewa na kocha msaidizi, John Tamba wakati wakisaka kocha mkuu mwenye sifa za kufundisha.
Naye Mohamed Rishard alisema kuwa kusitishiwa mkataba wake amelipokea kwa mikono miwili kutokana na timu kufanya vibaya kwani lilikuwepo moja ya kipengele kwenye mkataba kilitamka wazi endapo timu ingepoteza michezo mitatu kamati itamwita na kumhoji na wametekeleza kipengeleza
“Ni kweli mkataba
wangu wa kuifundisha Polisi Moro umesitishwa kutokana na timu kufanya vibaya na
nimeitwa na kamati utendaji na kuhojiwa kwanini timu inafanya vibaya nami
nimejieleza lakini kamati hiyo imefikia uamuzi wa kunisimamisha kazi na nimekubaliana
nao”, alisema Adolf.
Michezo ambayo Polisi Moro ilipoteza mfululizo Simba ambayo walifungwa mabao 2-0, Kagera
Sugar bao 1-0 na Mtibwa Sugar ambao waliilaza kwa mabao 2-1.
Pia Adolph alitoa tahadhari kwa kocha atayeridhi nafasi yake kujenga falsafa iliyo bora ili aivushe timu ili isishuke daraja maana yeye aliikuta timu ikiwa ina pointi nne na yeye amefikisha pointi ambazo haziwezi kuiondoa kwenye kushuka daraja na imebaki na michezo nane.
Pia Adolph alitoa tahadhari kwa kocha atayeridhi nafasi yake kujenga falsafa iliyo bora ili aivushe timu ili isishuke daraja maana yeye aliikuta timu ikiwa ina pointi nne na yeye amefikisha pointi ambazo haziwezi kuiondoa kwenye kushuka daraja na imebaki na michezo nane.
Kocha Mohamed Adolph Rishard alijiunga na klabu ya Polisi Moro wakati timu hiyo ikiwa ligi kuu Tanzania bara mzunguko wa pili msimu wa mwaka 2013/2014 na kushuka daraja kabla ya kurejea tena ligi kuu Tanzania bara msimu wa mwaka 2014/2015.
No comments:
Post a Comment