Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, October 3, 2014

NDUMBARU: UBABE WA MALINZI KWA BODI YA LIGI NA VILABU HAUVUMILIKI


Mwanasheria wa Vilabu Dr Damas Ndumbaru anasema Malinzi atasimamisha ligi kuu kwani vilabu havikubaliani na ubabe wake
Muda mfupi baada ya Rais wa shirikisho la soka nchini TFF Jamali Emily Malinzi kutangaza kuvibana vilabu vya ligi kuu kuchangia mapato yao kwa asilimia tano ili kuchangia miradi mbalimbali iliyo anzishwa na shirikisho la soka nchini, vilabu vya ligi kuu kupitia kwa mwanasheria wao Dr Damas Ndumbaru vimetishia kugomea kuendelea na ligi kuu ya soka inayoendelea hivi sasa na kumtaka Malinzi kuachana na agizo hilo ambalo linaonekana lina lengo la kuvinyonya zaidi vilabu.

Akiongea katika mazunguzo maalum na mtandao huu, Ndumbaru amesema tayari amezungumza na wateja wake ambao ni vilabu na wamekubaliana mambo kadhaa ikiwemo kuachana na ligi kuu pamoja na kuelekea shirikisho la soka duniani FIFA endapo Rais Malinzi atang'ang'nia msimamo huo.

No comments:

Post a Comment