Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 30, 2014

Alejandro Sabella amemtetea Lionel Messi licha ya kupondwa na Blatter


Bosi wa zamani wa Argentina Alejandro Sabella amemtetea mshambuliaji Lionel Messi akidai kuwa mshambuliaji huyo alijitoa kwa ajili ya taifa lake katika fainali ya kombe la dunia nchini Brazil.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 amekuwa katika mjadala mpana juu ya uwezo wake alionyesha katika fainali hizo zilizopita huku Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA Sepp Blatter hapo jana akikaririwa akisema kuwa mshambuliaji huyo hakustahili kushinda tuzo ya mpira wa dhahabu katika fainali hizo
Hata hivyo Sabella ameibuka na kudai kuwa Messi, ambaye ameshindwa kufunga goli baada ya kufunga magoli manne katika michezo mitatu alijotoa kwa kufanya kazi kubwa kwa ajili ya Argentina mpaka kuifikisha fainali alipokubali kucheza katika nafasi ya juu kwa kuwasaidia wachezaji wenzake.
"Messi ni mfano katika timu ya taifa," amesema Sabella mwenye umri wa miaka 59 alipokuwa akiongea na Radio La Red. "Alijitoa kimshikamano na wenzake
Sabella aliachia ngazi kuifundisha Argentina muda mfupi baada ya fainali hizo mjini Rio tangu kufikia mafanikio hayo ndani ya Albiceleste.

No comments:

Post a Comment