Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, July 15, 2013

MMILIKI MPYA WA FULHAM SHAHID KHAN ANATAKA KUIPELEA KLABU HIYO KATIKA KIWANGO KINGINE NA REAL MADRID YAMSAJILI ASIER ILLARRAMENDI

Mmiliki mpya wa klabu ya Fulham Shahid Khan ana matumaini ya kuijenga klabu hiyo kwa kufanyia kazi yale mtangulizi wake Mohamed Al Fayed.

Al Fayed mwenye umri wa miaka 84, aliinunua Fulham mwaka 1997 na kuifanya klabu hiyo kuwa moja ya klabu bora katika ligi kuu ya soka nchini England tangu mwaka 2001.Billionaire Khan ambaye ana umri wa miaka 62 kwasasa ameinunua klabu hiyo kutoka kwa Al Fayed ambapo amenukuliwa akisema klabu hiyo ni sehemu muafaka na eneo muhimu kwa wakati muafaka.

Mzaliwa huyo wa Pakistan alielekea nchini Marekeani wakati akiwa na umri mdogo wa miaka 16 na kuanza kujishughulisha na biashara ya spea za magari.Baadae akawa mmiliki wa timu ya NFL ya  Jacksonville Jaguars mwezi Desemba mwaka 2011 na sasa anakuwa mmiliki wa sita wa klabu kubwa nchini England inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini humo Premier League.

Fulham ilifikia katika hatua ya fainali ya michuano ya Europa chini ya meneja Roy Hodgson mwezi Mei mwaka 2010, ambapo walifungwa katika fainali na Atletico Madrid.Msimu uliopita ilikuwa chini ya meneja Martin Jol ambapo ilimaliza katika nafasi 12

Real Madrid yamsajili Asier Illarramendi kwa ada ya pauni milioni 34 akitokea Real SociedadReal Madrid imemsajili kiungo wa Real Sociedad Asier Illarramendi baada ya kukubali kulipa euro milioni 39 sawa na pauni milioni £34Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 anayechezea timu ya taifa ya Hispania ya vijana amesaini mkataba wa miaka sita na kuwa mmoja wa vijana wa the Bernabeu tayari amefanikiwa kupita katika vipimo vya afya.Illarramendi aliyetokea Sociedad, alikuwa msaada mkubwa katika klabu hiyo msimu uliopita ambapo aliiwezesha kumaliza katika nafasi ya nne na kupata nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa Ulaya.Pia amechezea michezo yote ya timu ya taifa ya vijana Hispania katika michuano ya European Under-21 nchini Israel mapema msimu huu wa kiangazi.Illarramendi anakuwa ni mchezaji wan ne kusajiliwa na kocha mpya wa Real Madrid Carlo Ancelotti baada ya kocha huyo kufanikisha usajili wa Isco aliyetokea Malaga kwa ada ya pauni milioni £23, Dani Carvajal aliyejiunga na klabu hiyo akitokea Bayer Leverkusen na Casemiro aliyejiunga na Madrid kwa mkopo akitokea Sao Paulo sasa akipewa mkataba wa kudumu.
 Alessandro Nesta aponda ligi kuu ya ItaliaMlinzi wa kati wa zamani wa kimataifa wa Italia Alessandro Nesta amesema ligi kuu ya soka nchini humo Serie A imeshindwa kufua dafu kwa ubora mbele ya ligi nyingine za barani Ulaya ikiwemo ligi ya Hispania, Ujerumani na England.Nesta ambaye kwasasa ana umri wa miaka 37 kwasasa anachezea soka katika klabu ya Montreal Impact inayoshiriki ligi kuu ya Marekani MLS.Akiwa bado nchini Italia Nesta aliwahi kushinda taji la Italia maarufu kama Scudetto mara tatu akiwa na vilabu vya Lazio na AC Milan.Nesta ametoa sababu ya kushindwa kwa ligi hiyo ya Italia na ligi nyingine ni kwamba kumetokana na kukosekana kwa fedha.Akinukuliwa amesema"Hakuna pesa kwasasa inchini Italia na hivyo wachezaji wazuri wamekuwa akikimbilia kucheza soka katika ligi za Hispania , England na Ujerumani. Ligi ina poromoka"Nesta, ambaye pia alishinda taji la kombe la dunia mwaka 2006, ameshangazwa na klabu ya Juventus kufanikiwa kumsajili mshambuliaji wa Manchester City Carlos Tevez kwa ada iliyotajwa kuwa ni pauni milioni £12.Amesema klabu hiyo imefanya usajili bora kwa kudaka saini ya Tevez, na kwamba hakuwahi kufikiria mchezaji kama Tevez kuelekea katika ligi ya Italia Serie A kwasasa. Amesema Juventus imefanya kazi kubwa.Nesta anataka kuelekea katika kazi ya ukocha itakapo fikiwa wakati wake wa kustaafu kucheza mwishoni mwa msimu ujao wa ligi kuu ya Marekani Major League Soccer .

No comments:

Post a Comment