Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 24, 2013

GERARDO MARTINO KUTOKA ARGENTINA HATIMAYE AVAA VIATU VYA TITO VILANOVA BARCELONA

RAIA wa Argentina, Gerardo Martino, Kocha wa Newell’s Old Boys ya huko Argentina, anatarajiwa kutangazwa kuwa Meneja mpya wa FC Barcelona kuchukua nafasi ya Tito Vilanova alieondoka kwa sababu za kiafya.


Martino, mwenye Miaka 50, anategemewa kusaini Mkataba wa Miaka mitatu na kutangazwa rasmi baadae Wiki hii.
Akiwa Nou Camp, Gerardo Martino atakuwa pamoja na Wasaidizi wake mwenyewe ambao ni Elvio Paolorrosso, Kocha wa Viungo, na Msaidizi Jorge Pautasso.

Awali ilitegemewa Kiungo wa zamani wa Barca, Luis Enrique, ndie atatwaa madaraka Nou Camp lakini tatizo kubwa ni kuwa Enrique alijiunga na Klabu ya La Liga Celta Vigo Mwezi uliopita tu na ukaja utata wa Mkataba.
Martino, au ‘Tata’ kama alivyo maarufu, anakuwa Muargentina wa nne kuwa Kocha wa Barcelona wengine ni Helenio Herrera, Roque Olsen na Cesar Luis Menotti na anatua Nuo Camp kuungana na Supastaa wa Argentina Lionel Messi ambae amemsifia sana Kocha huyu.
Jumatano, Barcelona inacheza Mechi ya Kirafiki na Mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich na itakuwa chini Jordi Roura kwenye Mechi hiyo iatakayochezwa huko Allianz Arena, Munich.

No comments:

Post a Comment